
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
NYOTA wawili wa kutumainiwa wa klabu ya Simba, Mlinda mlango Aishi Manula pamoja na kiungo mshambuliaji Shiza Kichuya, wamepokea viatu vyenye thamani ya Sh 500, 000 kutoka kwa mashabiki wa timu hiyo.
Wawili hao walikabidhiwa viatu hivyo aina ya CR7 Mercurial kutoka kampuni ya Nike, mara baada ya kumalizika kwa mchezo wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Lipuli, ulioisha kwa sare ya bao 1-1 uliopigwa katika Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.
Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa viatu hivyo, Manula alisema anajisikia fahari kupata zawadi hiyo kutoka kwa mashabiki hao ambao wameonyesha upendo wao kwake na kuahidi kuendelea kufanya vizuri ili kuwafurahisha zaidi.
βNi jambo zuri ambalo linatia hamasa ya kuendelea kujituma zaidi na kuisaidia timu kufanya vizuri zaidi katika michezo ya ligi kuu ili tuweze kutimiza malengo yetu,β alisema.
Naye Kichuya alisema zawadi hiyo itakuwa chachu kwake kufanya vizuri zaidi kutokana na upendo anaoonyeshwa na mashabiki hao, ambao wamekuwa wakiwaunga mkono katika harakati zao za kulisaka taji la Ligi Kuu ya Tanzania Bara.
Post A Comment: