
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
JESHI la Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, limelazimika kutumia mabomu ya machozi kutawanya kundi kubwa la wananchi waliozuia msafara wa Waziri Mkuu wa zamani na mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Edward Lowassa.
Maelfu ya wananchi hao walitawanywa jana kwa mabomu hayo baada ya kuziba barabara ya Soko la Mbuyuni eneo la Manyema wakati msafara wa Lowassa ukielekea Kata ya Bomambuzi, Manispaa ya Moshi.
Akizungumza na gazeti la Mtanzania, Katibu wa Chadema Mkoa wa Kilimanjaro, Basili Lema, alisema polisi walilazimika kurusha mabomu manne ya machozi ili kutawanya umati wa watu waliokuwa na shauku ya kumwona Lowassa.
βSaa 10:15 jioni katika Soko la Mbuyuni, polisi walirusha mabomu ya machozi ili kuwatawanya wananchi waweze kupisha msafara wa Lowassa kwa kuwa wengi wao waliziba kabisa barabara,β alisema.
Lema alisema kuwa Lowassa aliongozana na wabunge wawili wa chama hicho, Joshua Nasari na Esther Bulaya, kwenda kumnadi mgombea udiwani wa kata hiyo, Ninde Valerian.
Alisema baada ya polisi wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) kurusha mabomu hayo, wananchi walitawanyika na kuwezesha msafara huo kupita na kuelekea katika mkutano huo wa kampeni.
βBaada ya mabomu kurushwa, wananchi walitawanyika, tukaweza kuelekea katika mkutano wa hadhara na katika mkutano huo uliohudhuriwa na maelfu ya wananchi Lowassa alihutubia,β alisema.
Kwa upande wake, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Hamis Issah, alithibitisha polisi kurusha mabomu hayo na alisema walifanya hivyo ili kutawanya umati wa wananchi waliokuwa wamefunga barabara katika eneo la Manyema.
Post A Comment: