
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi 🇵🇪🇵🇪
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
SERIKALI imetenga Sh. bilioni 10 katika mwaka wa fedha 2017/18 kuwezesha upatikanaji wa dawa za kuzuia magonjwa nyemelezi.
Kauli hiyo ilitolewa mwishoni mwa wiki na Mkurugenzi Mkuu wa Bohari ya Dawa nchini (MSD), Laurean Bwanakunu, alipokuwa akiwasilisha taarifa ya utendaji wa bohari hiyo kwa kamati ya Bunge ya masuala ya Ukimwi.
Alisema hatua hiyo ya serikali imetokana na changamoto ya upatikanaji wa dawa hizo katika mwaka uliopita wa fedha kutokana na ufinyu wa bajeti ya serikali baada ya wafadhili kujitoa kununua dawa hizo.
“Serikali imetenga Sh. bilioni 10 ili kuwezesha upatikanaji wa dawa hizo na zitanunuliwa punde mgawo wa fedha utakapopatikana, hili limeenda sambamba na kuongeza ununuzi wa dawa za kawaida ambazo pia hutumia kwa kutibu magonjwa nyemelezi,”alisema Bwanakunu.
Aidha, alisema hali ya upatikanaji wa dawa za kufubaza makali ya virusi vya Ukimwi(ARVs) ni asilimia 100.
Post A Comment: