
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam kupitia Kikosi cha Usalama Barabarani kwa muda wa siku tano kupitia tozo za makosa barabarani, kimekusanya kiasi cha Sh. milioni 454.8
Kamanda wa Kanda hiyo, Lazaro Mambosasa, aliyasema hayo jana jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na waandishi wa habari.
Mambosasa alisema faini hizo zinatokana na operesheni ya ukamataji wa makosa mbalimbali ya barabarani kuanzia Alhamisi iliyopita hadi juzi.
Fedha hizo ukizigawa kwa siku maana yake ni kwamba jeshi hilo, lilikuwa likikusanya Sh. milioni 90.
Mambosasa alitaja idadi ya magari yaliyokamatwa kuwa ni 14,773, pikipiki 387, daladala 4,904, na magari mengine (binafsi na malori) ni 9,869.
Alisema idadi ya bodaboda waliofikishwa mahakamani kwa makosa ya kutovaa helmeti na kupakia mishikaki ni 26.
βJumla ya makosa yaliyokamatwa ni 15,160 na fedha za tozo zilizopatikana ni Sh. milioni 454.8,β alisema.
Pia alisema magari yaliyokamatwa kutokana na kuchelewa kulipa faini kwa wakati zaidi ya siku saba ni 1,846 ambapo kiasi kilicholipwa ni Sh. milioni 178.5.
Post A Comment: