Real Madrid imeweka wazi kwamba haitakuwa na huruma iwapo itashindwa kuidaka saini ya Harry Kane, kwani itapambana kumsajili mshambuliaji wa Manchester United, Marcus Rashford.



Awali, Rais wa Real Madrid, Florentino Perez aliweka wazi kwamba yupo tayari kumsajili Kane kwa gharama yoyote na ikishindwana naye, Rashford ndiye atakuwa mbadala.

Hata hivyo, mpango wa Real Madrid kumsajili Kane unaonekana kuingia dosari baada ya klabu hiyo kuweka wazi kwamba haipo tayari kumuuza na iwapo kuna klabu, iende na Pauni 200 milioni kwenye meza ya mazungumzo.

Perez alisema kwamba klabu hiyo ikimnasa Rashford jambo hilo litapokewa kwa shangwe na mashabiki wa klabu hiyo pia mchezaji, Cristiano Ronaldo.
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: