
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi 🇵🇪🇵🇪
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
Mwenyekiti wa CCM Taifa, Dkt. John Magufuli amemshukuru Rais Mstaafu Jakaya Kikwete kwa kutoangalia rushwa wala urafiki pindi alipomchagua kugombea urais na kutaka wanachama wake kuchagua wajumbe wa Halmashauri Kuu wenye mapenzi ya dhati na chama.
Dkt. Magufuli ameonya hayo wakati akifungua mkutano mkuu wa CCM mjini Dodoma jana ambapo amesema chama hicho kimedhamiria kupambana na rushwa na kwamba kama Rais Mstaafu Jakaya Kikwete angeangalia hayo basi yeye asingepata nafasi alonayo
“Msichague watu kwa urafiki au kwa sababu ya rushwa, binafsi napenda nimshukuru mzee Kikwete (Jakaya) yeye hakuangalia rushwa nadhani angefanya hivyo huenda mimi nisingepita,” amesema.
Aidha Dkt. Magufuli amewataka wanachama wa chama chake kuvunja makundi yaliyojitokeza wakati wa chaguzi wa ndani wa chama hicho.
“Vunjeni makundi chaguzi zimekiwasha tujikite kwenye kukiimarisha chama. CCM haitamvumilia mtu mwenye kuendeleza makundi,” amesema
Pamoja na hayo Dkt. Magufuli ameweka wazi hatosita kutengua matokeo ya uchaguzi wa wajumbe wa Halmashauri Kuu iwapo itabainika rushwa imetumika.
Post A Comment: