
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi 🇵🇪🇵🇪
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
MGOMBEA uenyekiti wa CCM Wilaya ya Babati, Elizabeth Malle, amewavunja mbavu wapigakura baada ya kujinadi wakati akiomba kura kuwa ana ujauzito wa mapacha.
Katika kinyang’anyiro hicho, Elizabeth alichuana na Andrew Ombay na Peter Mchuno na kuwashinda kwa kishindo.
Hata hivyo, alisema alikuwa anamaanisha akishinda uchaguzi huo atahakikisha anarejesha Jimbo la Babati Mjini na viti vya madiwani wa kata ambavyo vilienda upinzani.
Elizabeth alishinda kwa kupata kura 149 kati ya 282. Mpinzani mwenzake Ombay alipata kura 126 na Mchuno akiambulia kura nne.
Wagombea wote walikubali matokeo, lakini Ombay alilalamika kuwapo mchezo mchafu wa kunyimwa ushirikiano katika kata nyingine.
Alidai kulikuwapo na dalili za rushwa huku akiwaambia wajumbe kuwa kwa sababu ni mtoto wa mkulima na mfugaji hana fedha ndio maana amenyimwa kura.
Uchaguzi huo pia uliwapata viongozi wawakilishi wa wanawake, wajumbe wa Mkutano Mkuu Taifa, wawakilishi wa vijana, wajumbe wa mkutano mkuu mkoa, wajumbe wa Halmashauri Kuu Wilaya na Katibu Mwenezi.
Mapema Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Dk. Joel Bendera, aliwaangukia wajumbe huku akiwaomba wawachague viongozi makini ili waweze kuung’oa upinzani ambao amedai unampa aibu.
Akifungua mkutano mkuu wa uchaguzi wa wilaya hiyo na jimbo kwa ujumla watakaoongoza chama hicho kwa miaka mitano ijayo, Dk. Bendera aliwataka wajumbe kutofanya makosa katika uchaguzi huo.
“Mimi nimechoka na ninaona aibu kubwa kukaa mahali kwenye upinzani, naomba tutangulize hekima na busara ili kumpata kiongozi mzuri imani yako ndio ikuongoze kumpata kiongozi anayefaa,” alisema.
Aliwataka wajumbe wa mkutano huo kuhakikisha wanawachagua viongozi makini hata kama wapo ambao waliohongwa fedha wakawape watoto wao wakale, lakini wawachague viongozi wenye kuthubutu na siyo legelege.
“Mngejua tabu ninayoipata hapa mjini mimi na Mkuu wangu wa wilaya kuwaongoza wapinzani kwa kuwa wanapanga mambo yao, kuwabadilisha ni vigumu hivyo msituchagulie maharagwe na mbaazi ambao watashindwa kutuvusha,” alisema.
Msimamizi wa uchaguzi huo, Dk. Mary Nagu, aliwataka kuona umuhimu wa kuwa na viongozi imara ili waepuke kuongozwa na upinzani katika jimbo hilo.
Post A Comment: