
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
SERIKALI ya Cuba imejenga mnara wa kumbukumbu ya mashujaa wa ukombozi wa Afrika, akiwamo baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, ikiwa sehemu ya kutambua mchango wao.
Kutokana na hatua hiyo, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, ameishukuru serikali ya Cuba kwa kutambua na kuthamini mchango mkubwa uliotolewa na mashujaa wa ukombozi wa bara la Afrika.
Mnara huo umejengwa katika Manispaa ya Playa, jijini Havana kwenye eneo maalum la makumbusho ya mashujaa walioshiriki katika ukombozi wa Afrika na kuwekwa sanamu zao na maelezo mafupi ya historia zao na nchi wanazotoka.
Waziri Mkuu alifanya ziara katika eneo hilo juzi na kuweka shada la maua katika mnara huo uliozungukwa na sanamu za mashajuaa wa bara la Afrika na kuonyeshwa sehemu itakayowekwa sanamu ya Mwalimu Nyerere.
Akiwa katika eneo hilo, Waziri Mkuu aliishukuru serikali ya Cuba kwa kujenga makumbusho ya mashujaa hao na kwamba serikali ya Tanzania itashirikiana na Cuba kuhakikisha kuwa sanamu ya Mwalimu Nyerere inawekwa katika sehemu iliyotengwa.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Taasisi ya Ushirikiano wa Cuba na Nchi Marafiki, Joseβ Prieto Cintado, alisema mnara huo umejengwa kwa lengo la kutambua thamani na umuhimu wa viongozi hao.
Mkurugenzi huyo alisema serikali ya Cuba inathamini mchango mkubwa uliotolewa na mashujaa hao katika vita ya ukombozi wa Afrika, hivyo iliamua kujenga mnara wa kumbukumbu katika nchi yao.
Alisema wananchi wa Cuba na watu kutoka mataifa mbalimbali ndani na nje ya Afrika, wanakwenda katika eneo hilo la makumbusho na kujifunza historia za viongozi hao. Pia eneo hilo linatumiwa na watafiti wa masuala ya kihistoria.
Mashujaa ambao tayari sanamu zao zimekwishawekwa kwenye eneo la kuzunguka mnara huo ni marais wa kwanza Jomo Kenyatta (Rais wa kwanza wa Kenya), Modibo Keita (Mali) na Amilcar Cabral (Guinea Bissau).
Wengine ni Dk. Kwame Nkrumah (Ghana), Oliver Thambo (Kiongozi Mwandamizi wa Chama cha Ukombozi cha ANC cha Afrika Kusini), Eduardo Mondlane (Kiongozi wa ukombozi nchini Msumbuji) na Samora Machel (Rais wa kwanza wa Msumbuji).
Wengine ni Sekou Toure (Guinea), Seretse Khama (Botswana), Alhaji Aboubakar Tafawa Balewa na Obafemi Jeremiah Awolowo (Mawaziri Wakuu wa zamani wa Nigeria) na Chifu Jeremia Azikiwe (Rais wa zamani wa Nigeria).
Post A Comment: