
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
Katika hali isiyokuwa ya kawaida, mtoto wa miaka miwili Buyunga Baragi amekutwa akiwa amechinjwa, huku panga lenye matone ya damu likiwa ndani ya nyumba anayoishi.
Mtoto huyo, mkazi wa Kijiji cha Iharara, wilayani hapa Mkoa wa Mara, alichinjwa akiwa amelala chumbani pamoja na watoto wenzake.
Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji hicho, Makuru Siboti alisema tukio hilo lilitokea juzi saa 12 :30 jioni na kuibua hofu na simanzi miongoni mwa wakazi wa eneo hilo.
Mkuu wa Upelelezi Wilaya ya Serengeti, Alfred Kyeba aliyeongoza kikosi cha uchunguzi alithibitisha kutokea kwa tukio hilo.
Akizungumza kifo cha mjukuu wake, Bendu Baragi alisema tukio hilo liligundulika baada ya wazazi kurejea nyumbani kutoka kwenye shughuli zao za kila siku.
Baragi alisema aliyebaini mauaji hayo ni mama wa marehemu, Silya Fadhili aliyekuwa ametoka kuchunga mifugo yake na kuwakuta watoto wake wamelala lakini alipowaangalia vizuri aligundua mmoja wao alikatwa shingo.
"Polisi wamefika hapa nyumbani na kuondoka na baba wa marehemu pamoja na shangazi yake baada ya panga lenye matone ya damu kukutwa ndani ya nyumba ya familia", alisema Baragi.
Hili ni tukio la pili la mtu kuuawa kwa kuchinjwa wilayani Serengeti, likitanguliwa na lile mkazi wa Kitongoji cha Mariwa, Kijiji cha Nyiberekera, Teksi Ngiteli (21), aliyekutwa amechinjwa nyumbani kwao.
Chanzo: Mwananchi
Post A Comment: