
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi 🇵🇪🇵🇪
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
MBUNGE wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (Chadema) jana alihojiwa na
Polisi jijini Dar es Salaam kwa saa sita, kuhusu mkutano wake na
wanahabari wiki iliyopita kuzungumzia kupotea kwa Ben Saanane.
Saanane ni Mkuu wa Idara ya Utafiti na Sera wa Chadema na msaidizi wa
Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe na ilielezwa alipotea tangu
Novemba 14 mwaka huu na mpaka sasa haijajulikani alipo.
Akizungumza jana, Lissu alisema hakukamatwa, bali aliitwa kuhojiwa kuhusu mkutano wake na wanahabari wiki iliyopita.
“Sijakamatwa ila nimeitwa kuhojiwa kuhusu ile ‘Press Conference’
(mkutano na waandishi wa habari) ya wiki iliyopita na nimetakiwa nitoe
maelezo kuhusu Saanane. “Nilitakiwa nifike polisi saa mbili asubuhi
kituo cha kati (kituo kikuu).
Nimefika saa nne kuhojiwa kuhusu mambo
mawili; moja nitoe ushahidi kuhusu kupotea kwa Ben Saanane na kauli
zilizoitwa za uchochezi nilizozitoa katika mkutano wangu na waandishi wa
habari,” alisema Lissu aliyehojiwa hadi saa kumi jioni.
Hivi karibuni, Lissu alisema Chadema haifahamu alipo Saanane na
kuitaka serikali ieleze mahali alipo msaidizi huyo wa Mbowe kwa kuwa
moja ya kazi za chombo hicho ni kulinda raia wake.
Hata hivyo, juzi Kaimu Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai,
Robert Boaz, alisema Polisi haijui alipo Saanane na inaendelea na
uchunguzi wa kina kubaini alipo kiongozi huyo wa Chadema.
Aidha, alieleza kuendelea na uchunguzi wa miili saba iliyokutwa kando
ya Mto Ruvu wilayani Bagamoyo ikiwa imefungwa katika mifuko ya
sarandusi.
DOWNLOAD
APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA
KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD
BONYEZA HAPA
ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
Post A Comment: