Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais John Magufuli imepongezwa kwa kuongoza vyema nchi kwa utulivu na amani kwa kuendelea kuwaunganisha waumini wa dini zote, Waislamu na Wakristo.


Akitoa salamu za Sikukuu ya Krismasi Dar es Salaam jana, Kiongozi Mkuu wa Waislamu wa Dhehebu la Shia, Shehe Hemed Jalala alisema kuwa wanaendelea kuombea amani ya nchi pamoja na viongozi wote ili wapate hekima na busara ya kuendelea kuongoza vyema.

“Ninamuomba Mwenyezi Mungu kupitia Serikali hii awape hekima na busara viongozi wetu ili waendelee kutuongoza kwa salama na amani na vilevile wazidi kuboresha maelewano kati yetu sisi Waislam na ndugu zetu wakristo,” alisema Shehe Jalala.

Pia alisema kuwa mtu yeyote ambaye ana nia ya kuleta chokochoko ya kuvunja amani hiyo, asiweze kuingia katika nchi ya Tanzania ili Taifa lizidi kuwa na amani kwa ajili ya ustawi wake.

Hata hivyo, alisema kuwa salamu hizo kwa wakristo wote nchini na duniani ni kuonesha kwamba Uislam hauna chinja chinja wala ukatili kwa Wakristo, badala yake ni kudumisha amani na maelewano kati yao.

Alifafanua kuwa Waislamu na Wakristo wote ni ndugu, ambao wanaamini kwa Mungu mmoja na kwamba wote wanapaswa kuilinda amani ya Tanzania.

“Sisi Waislamu na Wakristo sote ni Watanzania ni wajibu wetu kuwa na umoja na mshikamano ni makosa makubwa kufungua mwanya wowote wa mvutano kati ya Waislam na Wakristo hapa Tanzania,” alisema.

Alisema ni vyema kuvumiliana kupitia tofauti za itikadi, mitazamo na fikra, ili kuepusha kugawanyika. Alisema Watanzania tukiendelea kuipenda nchi, amani itaimarika.

Aidha, alisisitiza kuwa salamu za Krismasi zinaonesha ishara ya upendo kwa ndugu zao Wakristo, kwa kuwa katika Vitabu Vitakatifu vinahamasisha kupendana kama mtu apendavyo nafsi yake na kwamba hakuna uadui kati ya dini hizo.

“Niwatakie mkono wa pongezi ndugu zetu Wakristo kwa kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Nabii Issa (Yesu Kristo),” alisema.

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: