
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi 🇵🇪🇵🇪
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais John Magufuli imepongezwa
kwa kuongoza vyema nchi kwa utulivu na amani kwa kuendelea kuwaunganisha
waumini wa dini zote, Waislamu na Wakristo.
Akitoa salamu za Sikukuu ya Krismasi Dar es Salaam jana, Kiongozi
Mkuu wa Waislamu wa Dhehebu la Shia, Shehe Hemed Jalala alisema kuwa
wanaendelea kuombea amani ya nchi pamoja na viongozi wote ili wapate
hekima na busara ya kuendelea kuongoza vyema.
“Ninamuomba Mwenyezi Mungu kupitia Serikali hii awape hekima na
busara viongozi wetu ili waendelee kutuongoza kwa salama na amani na
vilevile wazidi kuboresha maelewano kati yetu sisi Waislam na ndugu zetu
wakristo,” alisema Shehe Jalala.
Pia alisema kuwa mtu yeyote ambaye ana nia ya kuleta chokochoko ya
kuvunja amani hiyo, asiweze kuingia katika nchi ya Tanzania ili Taifa
lizidi kuwa na amani kwa ajili ya ustawi wake.
Hata hivyo, alisema kuwa salamu hizo kwa wakristo wote nchini na
duniani ni kuonesha kwamba Uislam hauna chinja chinja wala ukatili kwa
Wakristo, badala yake ni kudumisha amani na maelewano kati yao.
Alifafanua kuwa Waislamu na Wakristo wote ni ndugu, ambao wanaamini
kwa Mungu mmoja na kwamba wote wanapaswa kuilinda amani ya Tanzania.
“Sisi Waislamu na Wakristo sote ni Watanzania ni wajibu wetu kuwa na
umoja na mshikamano ni makosa makubwa kufungua mwanya wowote wa mvutano
kati ya Waislam na Wakristo hapa Tanzania,” alisema.
Alisema ni vyema kuvumiliana kupitia tofauti za itikadi, mitazamo na
fikra, ili kuepusha kugawanyika. Alisema Watanzania tukiendelea kuipenda
nchi, amani itaimarika.
Aidha, alisisitiza kuwa salamu za Krismasi zinaonesha ishara ya
upendo kwa ndugu zao Wakristo, kwa kuwa katika Vitabu Vitakatifu
vinahamasisha kupendana kama mtu apendavyo nafsi yake na kwamba hakuna
uadui kati ya dini hizo.
“Niwatakie mkono wa pongezi ndugu zetu Wakristo kwa kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Nabii Issa (Yesu Kristo),” alisema.
DOWNLOAD
APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA
KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD
BONYEZA HAPA
ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
Post A Comment: