
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi 🇵🇪🇵🇪
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
WAKRISTO nchini wameaswa kuunga mkono juhudi za Rais John Magufuli za
kupiga vita ubinafsi ili kujenga nchi yenye upendo, amani na maendeleo.
Mwito huo umetolewa na Askofu wa Kanisa la Moravian, Jimbo la
Mashariki na Pwani Tanzania, Emmaus Bandekile Mwamakula jana katika
salamu zake kwa wakristo za Sikukuu ya Krismasi na Mwaka Mpya.
“Tunaposherehekea sikukuu ya Krismasi hatuna budi kukumbuka maana
halisi ya Krismasi. Biblia inafundisha kuwa Yesu Kristo aliamua kuacha
utukufu wote aliokuwa nao mbinguni pale alipozaliwa sehemu ya kulishia
ng’ombe ili awatumikie na kuwakomboa wanadamu,” alisema Askofu
Mwamakula.
Alisema tukio la kumbukizi ya kuzaliwa Yesu Kristo linawakumbusha
Wakristo kuacha ubinafsi na kwani hakuna jamii yoyote iliyofanikiwa
popote duniani kama inaendeleza ubinafsi.
Askofu Mwamakula alisema vita dhidi ya ubinafsi inayopigwa kwa nguvu
zote na Rais Magufuli, inapaswa kuungwa mkono kwani ubinafsi ni adui wa
haki, upendo, umoja, amani na maendeleo.
"Ubinafsi unafanya hospitali zinakosa dawa na huduma muhimu na
kusababisha watu ambao wangekuwa wazalishaji mali kupoteza maisha
kwasababu tu watu wachache wametumia pesa zilizotakiwa kutumika
kuwatibia,” alisema askofu huyo.
Alisema Rais Magufuli ametambua madhara ya ubinafsi ndio maana
ameanzisha vita alivyovipa jina la “Kutumbua Majipu” hivyo anapaswa
kuungwa mkono na kupongezwa.
Aliwasihi Watanzania wote kuungana kwa kuwa vita hivyo havina dini,
kabila, itikadi, jinsia, umri wala rangi na kuongeza kuwa kama jamii
inahitaji demokrasia ya kweli, ni lazima kupiga vita ubinafsi.
DOWNLOAD
APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA
KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD
BONYEZA HAPA
ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
Post A Comment: