
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
HUKUMU ya mwanamume nchini Malawi aliyesema amefanya ngono na
wasichana na wanawake takribani 104 kama sehemu ya kuwatoa nuksi huku
akijua kwamba anaishi na virusi vya Ukimwi (VVU) inatarajiwa kutoka
wakati wowote.
Mtu huyo alikamatwa baada ya kufanya mazungumzo ya kina na Shirika la
Utangazaji la Uingereza kuhusu ufanyaji huo mapenzi wenye lengo la
kuondoa nuksi kwa wanawake na pia kuwaingiza ukubwani mabinti.
Mwanamume huyo Eric Aniva alikamatwa nyumbani kwake Julai mwaka huu
baada ya kukiri kwamba alifanya mapenzi na mabinti ambao wengine
walikuwa ni watoto wa miaka 12 huku akijua kwamba anaishi na VVU.
Aidha, hali yake hiyo hakuwahi kumweleza mtu yeyote aliyekuwa anamtumia kama sehemu ya utamaduni wa eneo analotoka.
Aniva anasema kwamba alikuwa anakodishwa na ndugu wa mabinti hao
kufanya nao ngono kama sehemu ya kuwaingiza ukubwani na wakubwa
kuwaondoa nuksi hasa waliofiwa.
Inaaminika kwamba kama mwanamke aliyefiwa hatafanyiwa matendo hayo
anaweza kuandamwa na bahati mbaya, kifo cha ghafla na hata ugonjwa.
Wakati Rais wa Malawi, Peter Mutharika alipotoa agizo la Aniva
akamatwe na ashitakiwe kwa kubaka hakuna msichana aliyejitokeza kutoa
ushahidi dhidi yake.
Kutokana na mazingira hayo, alibadilishiwa mashtaka na kushtakiwa kwa
kujihusisha na utamaduni ambao ni hatarishi kwa mujibu wa kifungu cha
tano cha sheria ya usawa wa jinsia ambapo alituhumiwa kufanya mapenzi na
wajane.
Katika shitaka hili wanawake wawili wamejitokeza kutoa ushahidi dhidi
ya Aniva ambapo mmoja alisema alifanyiwa kitendo hicho kabla ya matendo
hayo kupigwa marufuku huku mwingine akisema alifanikiwa kutoroka kabla
ya kuingiliwa kimwili.
DOWNLOAD
APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA
KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD
BONYEZA HAPA
ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
Post A Comment: