
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi 🇵🇪🇵🇪
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
Robert Mugabe alijiuzulu Novemba 21 baada ya kuahidiwa kinga ya kutoshtakiwa, kulipwa dola za Marekani 10 milioni kwa mkupuo, mshahara wa kila mwezi, matibabu, usalama wake pamoja na ulinzi wa mali zake, gazeti la Independent limeandika.
Uchunguzi uliofanywa na Independent umefichua kwamba watu wa Mugabe walioshiriki katika mazungumzo yaliyowezesha yeye kuondoka walifanikiwa kufikia makubaliano na majenerali kuhakikisha mkongwe huyo mwenye umri wa miaka 93 haendi kuishi uhamishoni bali afurahie kustaafu kwake nchini Zimbabwe na apate marupurupu yake.
“Serikali itamlipa Mugabe dola 5 milioni kwa mkupuo na kisha kiasi kinachosalia atakuwa akilipwa kwa mafungu,” chanzo kimoja kimesema. “Mugabe atapatiwa matibabu pamoja na mshahara kamili kila mwezi. Na ikiwa atafariki mkewe atakuwa analipwa nusu mshahara kila mwezi.”
Mugabe alifanya majadiliano ili aweze kuondoka salama kupitia timu ya wapatanishi ambayo ilijumuisha kasisi wa Kikatoliki, Fidelis Mukonori na gavana wa zamani wa RBZ Gideon Gono. Mukonori alisema katika mahojiano kwamba wajibu wake ulikuwa kuwa mpatanishi kati ya majenerali na Mugabe.
Post A Comment: