
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
KOCHA Mkuu wa Yanga, Hans van Pluijm amesema timu yake haijashuka
kiwango kama ambavyo baadhi ya wadau wa soka wanavyodai na kuongeza kuwa
muda si mrefu watarudi katika ubora wao.
Baadhi ya wadau na wachambuzi wa soka kwa siku za karibuni wamekuwa
wakitoa maoni yao kuwa Yanga imekwisha na wengine wakidai imechoka
kutokana na wachezaji wengi kutopata muda wa kupumzika baada ya kutoka
kwenye mashindano ya kimataifa.
Akizungumza na gazeti hili jana, Pluijm alisema muda sio mrefu watarudi tena na itadhihirika kama kweli wamechoka ama la.
βSio kweli kama tumekwisha, tuko vizuri na muda sio mrefu mtaona
mambo mazuri, tunaendelea kujipanga na kurekebisha mapungufu yetu
kuhakikisha tunafanya vizuri,βalisema.
Yanga imetoka kulazimishwa sare ya bao 1-1 dhidi ya Simba katika
mchezo uliochezwa kwenye uwanja wa Taifa, Dar es Salaam mwishoni mwa
wiki iliyopita.
Matokeo hayo yameishusha kutoka nafasi ya tatu hadi ya tano ikiwa na
pointi 11 sawa na Azam FC ambao wanashika nafasi ya sita, lakini Yanga
ikiwa nyuma mchezo mmoja.
Timu zinazoongoza nne bora ni Simba yenye pointi 17, Stand United 15, Mtibwa Sugar 13 na Kagera Sugar yenye pointi 12.
DOWNLOAD
APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA
KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD
BONYEZA HAPA
ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
Post A Comment: