
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Mbeya, imemhukumu mtoto wa Mbunge wa
Mbarali, Haroon Mulla Pirmohamed (CCM) kulipa faini ya Sh138,390,000 au
kifungo cha miaka 20 jela, baada ya kukiri kosa na kutiwa hatiani kwa
kumiliki nyara mbalimbali za Serikali.
Katika kesi hiyo, mtoto huyo Pirmohamed Haroon alikutwa akimiliki kilo 46 za nyama ya tandala, mbawala, swala pala, tohe, njiwa pori, kanga pori na pembe za tandala na tohe vyote vikiwa na thamani ya Sh138,390,000.
Akisoma hukumu, Hakimu Mkazi Mwandamizi wa Mahakama hiyo, Michael Mteite alimhukumu mshtakiwa huyo kulipa faini hiyo ambayo ni mara 10 ya thamani ya nyara alizokutwa nazo na iwapo atashindwa atumikie kifungo cha miaka 20.
Hata hivyo, baada ya kutolewa kwa hukumu hiyo, Haroon alikwepa adhabu ya kifungo kwa kulipa kiasi hicho cha fedha na kupatiwa risiti ya malipo ya Serikali namba 8870022.
DOWNLOAD
APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA
KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD
BONYEZA HAPA
ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
Post A Comment: