
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira, imetangaza
kutoshirikiana na Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira kwa kuwa
imekuwa ikifanya mambo yake bila kuishirikisha.
Mambo hayo ni
pamoja na kuendesha bomoabomoa ya nyumba za mabondeni na kufanya ziara kwenye
maeneo ya migodi.
Mbali na hilo imegoma pia kujadili taarifa ya utupaji taka kwenye migodi iliyokuwa iwasilishwe na Ofisi hiyo, kwa madai kuwa kazi yao si kujadili taarifa wasiojua uhalisia wake.
Wakizungumza hapa jana, wajumbe wa Kamati hiyo walisema, Kamati yao ni nyeti hivyo inapaswa kutengewa fedha za kutosha, ili itembelee maeneo mbali mbali yakiwamo ya migodi ili kujionea utupaji taka na bomoabomoa mabondeni jambo ambalo walisema Ofisi hiyo haiipi ushirikiano.
Mbunge wa
Monduli, Julius Kalanga (Chadema) alisema inasikitisha kuona Serikali yenye
kaulimbiu ya Hapa Kazi Tu, inabana matumizi hadi kwa wabunge ambao wanafanya
kazi zake.
"Si kwamba sisi wabunge tunakubaliana na matumizi mabaya ya fedha za Serikali, lakini haiwezekani wabunge walio kwenye Kamati nyeti ya mazingira, wananyimwa fedha za kutembelea maeneo ambayo yanaonekana kuwa na mkanganyiko kwa nia ya kuishauri Serikali,β alisema.
"Hii Kamati si ya kujadili taarifa tu kwa lengo la kuishauri Serikali bila kufika sehemu husika ili kujiridhisha," alisema Mbunge huyo.
Mbunge wa Viti
Maalumu,Thauhida Nyimbo (CCM) alisema wabunge hawapo kwa ajili ya kufanya kazi
za Serikali, wala kufurahisha mawaziri na timu zao, bali kusimamia
Serikali kwa maslahi ya wananchi.
βHivi hapa Naibu Waziri na timu yako mnatuletea hii taarifa tujadili kitu gani au nyie Wizara hamjui wajibu wenu? Hivi kweli mnadhani sisi hapa ni wasaidizi wenu au tunafanya kazi za Serikali? Kazi yetu ni kuishauri Serikali na si kufanya kazi za Serikali,β alisema.
Mbunge wa
Konde, Khatibu Haji Kombo (CUF) alisema kama Kamati haitakuwa karibu na Wizara,
kwa maana ya kufanya ziara katika maeneo yenye migogoro ni bora isifanye jambo
lolote na Wizara hiyo.
Alisema inakuwaje masuala muhimu kama sumu za taka katika maeneo ya migodi na sehemu za bomoabomoa mabondeni, wabunge wa Kamati husika wasiende kujionea kinachofanyika na kuhoji wananchi ili kupata picha kamili.
Mbunge wa Moshi Mjini, Anthony Komu (Chadema) aliunga mkono kukataliwa taarifa ya Ofisi ya Makamu wa Rais, Mazingira, kwa madai kuwa wakiijadili watakuwa hawatendei haki wananchi.
DOWNLOAD
APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA
KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD
BONYEZA HAPA
ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
Post A Comment: