KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira, imetangaza kutoshirikiana na Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira kwa kuwa imekuwa ikifanya mambo yake bila kuishirikisha.



Mambo hayo ni pamoja na kuendesha bomoabomoa ya nyumba za mabondeni na kufanya ziara kwenye maeneo ya migodi.

Mbali na hilo imegoma pia kujadili taarifa ya utupaji taka kwenye migodi iliyokuwa iwasilishwe na Ofisi hiyo, kwa madai kuwa kazi yao si kujadili taarifa wasiojua uhalisia wake.

Wakizungumza hapa jana, wajumbe wa Kamati hiyo walisema, Kamati yao ni nyeti hivyo inapaswa kutengewa fedha za kutosha, ili itembelee maeneo mbali mbali yakiwamo ya migodi ili  kujionea utupaji taka na bomoabomoa mabondeni jambo ambalo walisema Ofisi hiyo haiipi ushirikiano.  

Mbunge wa Monduli, Julius Kalanga (Chadema) alisema inasikitisha kuona Serikali yenye kaulimbiu ya Hapa Kazi Tu, inabana matumizi hadi kwa wabunge ambao wanafanya kazi zake.

"Si kwamba sisi wabunge tunakubaliana  na matumizi mabaya ya fedha za Serikali, lakini haiwezekani wabunge walio kwenye Kamati nyeti ya mazingira, wananyimwa fedha za kutembelea maeneo ambayo yanaonekana kuwa na mkanganyiko kwa nia ya kuishauri Serikali,” alisema.

"Hii Kamati si ya kujadili taarifa tu kwa lengo la kuishauri Serikali bila kufika sehemu husika ili kujiridhisha," alisema Mbunge huyo.

Mbunge wa Viti Maalumu,Thauhida Nyimbo (CCM) alisema wabunge hawapo kwa ajili ya kufanya kazi za Serikali,  wala kufurahisha mawaziri na timu zao, bali kusimamia  Serikali  kwa maslahi  ya wananchi.

β€œHivi hapa Naibu Waziri na timu yako mnatuletea hii taarifa   tujadili kitu gani au nyie Wizara hamjui wajibu wenu? Hivi kweli mnadhani sisi hapa ni wasaidizi wenu au tunafanya kazi za Serikali? Kazi yetu ni kuishauri Serikali na si kufanya kazi za Serikali,” alisema.

Mbunge  wa Konde, Khatibu Haji Kombo (CUF) alisema kama Kamati haitakuwa karibu na Wizara, kwa maana ya kufanya ziara katika maeneo yenye migogoro ni bora isifanye jambo lolote na Wizara hiyo.

Alisema inakuwaje masuala muhimu kama sumu za taka katika maeneo ya migodi na sehemu za bomoabomoa mabondeni, wabunge wa Kamati husika wasiende kujionea kinachofanyika  na kuhoji wananchi ili kupata picha kamili.

Mbunge wa Moshi Mjini, Anthony Komu (Chadema) aliunga mkono kukataliwa taarifa ya Ofisi ya Makamu wa Rais, Mazingira, kwa madai kuwa wakiijadili watakuwa hawatendei haki wananchi.
 
DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: