
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi 🇵🇪🇵🇪
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
MTU anayepata fursa ya kufika nchini Senegal, Afrika Magharibi, ni
vyema pia akakitembelea kisiwa cha Gorée kilichopo kilomita tatu kutoka
pwani ya Jiji la Dakar ambapo, miongoni mwa mambo mengine, ataona kile
kiitwacho kwa Kiingereza ‘Door of No Return’ yaani mlango ambao
ukishaupita hutaweza kurejea tena.
Mlango huo upo katika jengo kubwa la zamani lijulikanano kama ‘House
of Slaves’ au Jumba la Watumwa. Kwa Kifaransa linaitwa ‘Maison des
Esclaves’. Mlango huo ulikuwa ndiyo mapito ya mwisho ya Waafrika
waliokuwa wanasombwa kwa mamilioni kwenda utumwani sehemu mbalimbali
duniani, hususani Bara la Amerika.
![]() |
Rais Barack Obama na mkewe wakiwa ‘Door of No Return’ walipotembelea kisiwa cha Gorée Juni 27, 2013. |
Kwa mtumwa ukiupita mlango huo basi unaelekea moja kwa moja kwenye
majahazi au meli zilizokuwa zimetia nanga na kuanza safari ya maelfu ya
maili kwenda utumwani ambako walilowea kwenda kufanyishwa kazi kwa
nguvu, wakafia huo na kuacha vizazi ambavyo hadi leo vipo Marekani,
Uingereza, Cuba na kadhalika.
Jengo hilo lililokarabatiwa kidogo, lilijengwa mnamo 1776 na
kuendelea kuweka namba kubwa ya watumwa hadi mwanzoni mwa miaka ya 1800,
pamoja na takwimu zinazokinzana hasa kutoka kwa Wazungu, mlango wake
unaaminika ulipitisha Waafrika zaidi ya milioni 15 kwenda utumwani
hususan Amerika.
![]() |
Obama akiangalia mandhari ya eneo hilo. |
Jumba hilo pamoja na kuwa kivutio cha kusikitisha kwa Waafrika,
limetembelewa na watu kibao duniani wakiwemo Papa John Paul wa Pili,
Rais Barack Obama, na marehemu Nelson Mandela ambaye kufika kwake hapo
kulimtoa machozi hadharani.
DOWNLOAD
APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA
KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD
BONYEZA HAPA
ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
Post A Comment: