
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi 🇵🇪🇵🇪
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
HASHIM Rungwe, Mwenyekiti wa Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA),
amesema chama hicho kipo mbioni kujiunga na vyama vinavyounda Umoja wa
Katiba ya Wananchi (UKAWA) wakati wowote kuanzia sasa.
Rungwe ambaye pia alikuwa mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CHAUMMA katika uchaguzi mkuu wa mwaka jana, amesema kuwa hakuna mtu yoyote timamu anayeweza kubeza mafanikio ya muungano wa vyama vya UKAWA.
“UKAWA imeleta mafanikio makubwa sana kwa vyama vya upinzani, hakuna mtu aliye timamu anaweza kubeza hilo. Sisi kama CHAUMMA, tupo kwenye mchakato wa kuangalia namna ya kuunganisha nguvu na UKAWA,” amesema Rungwe.
Rungwe alikuwa akizungumza asubuhi ya leo katika kipindi cha Power Breakfast, ambacho hurushwa na kituo cha Clouds Fm. Pamoja na mambo mengine pia ameelezea namna alivyokuwa akimuombea kura mgombea Urais wa CHADEMA, aliyekuwa akiungwa mkono na vyama vya UKAWA katika uchaguzi mkuu wa mwaka jana.
“Licha ya mimi kugombea urais, lakini kila nilipopita katika mikutano yangu nilikuwa nikiwambia wananchi, kama wanaona mimi sifai kuwa rais wa nchi basi wamchague mgombea wa UKAWA, mimi nilikuwa nikipambana na Chama Cha Mapinduzi tu,” amesema.
Alipoulizwa, kwanini chama chake kiliamua kusimamisha mgombea ilihali kilikuwa na imani na mgombea urais wa UKAWA, Rungwe amesema CHAUMMA kilikuwa chama kipya kilichohitaji kujitambulisha kwa watanzania.
“Chama cha siasa hakiendeshwi kwa one man show (uamuzi wa mtu mmoja), bali kwa maamuzi ya vikao vya chama, kwa kuwa sisi tulikuwa bado chama kipya cha siasa tuliamua tusimamishe mgombea urais na kwakweli tumefanikiwa kujitambulisha,” amesema.
DOWNLOAD
APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA
KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD
BONYEZA HAPA
ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
Post A Comment: