
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi 🇵🇪🇵🇪
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk Ali Mohamed
Shein ameiagiza Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu Zanzibar kupitia Wizara
ya Elimu na Mafunzo ya Amali, kusimamisha utoaji wa mikopo ya elimu ya
juu, hadi hapo serikali itakapojiridhisha na utaratibu mzima wa utoaji
wa mikopo hiyo.
“Hatutatoa mikopo mwaka huu mpaka hapo tutakapokamilisha kazi ambayo
tumeanza kuifanya ya kupitia upya utaratibu wa utoaji mikopo hiyo ili
kuhakikisha inatolewa kulingana na mahitaji ya sasa ya nchi na kwa
wanaostahili,” alisema Dk Shein.
Akizungumza katika hafla ya utoaji zawadi kwa wanafunzi waliofaulu
daraja la kwanza katika mitihani ya Taifa ya Kidato cha Nne mwaka 2015
na Kidato cha Sita mwaka 2016, Dk Shein alisema kuwa katika utaratibu wa
sasa wapo waliodanganya kupata mikopo na ambao wamekopeshwa lakini
wamekuwa wagumu kurejesha mikopo hiyo.
Katika hafla hiyo, ambayo ilihudhuriwa pia na Waziri wa Nchi, Ofisi
ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Issa Haji Usii Gavu, jumla
ya wanafunzi 119 waliomaliza kidato cha nne na wengine 50 waliomaliza
kidato cha sita, walipewa zawadi kwa kupata daraja la kwanza katika
mitihani yao ya taifa.
“Wako waliokejeli matokeo yenu, lakini ukweli ni huo mko 50 wa kidato
cha tano mliopata daraja la kwanza na wengine 119 mliofaulu daraja la
kwanza mtihani wa kidato cha nne,” alieleza Dk Shein na kuhoji msingi wa
kukebehi matokeo hayo.
DOWNLOAD
APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA
KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD
BONYEZA HAPA
ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
Post A Comment: