
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi 🇵🇪🇵🇪
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
JESHI la Polisi limekwama kumhoji Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (Chadema), akiwa hospitalini Nairobi, Kenya.
Taarifa iliyotolewa na Lissu jana ilisema polisi wa Tanzania hawawezi kumhoji akiwa nchini Kenya au kwingineko nje ya mipaka ya nchi.
Kauli ya Lissu imekuja siku 10 tangu Mkuu wa Jeshi la Polisi, IGP Simon Sirro, kusema kuwa wametuma askari wawili kwenda Nairobi kuchukua maelezo ya Lissu, baada ya Mbunge huyo kukubali kuhojiwa.
Lissu alishambuliwa kwa risasi 32 na watu wasiojulikana mchana wa Septemba 7, mwaka huu nje ya nyumba yake Area D mjini Dodoma, wakati akitoka bungeni kwa mujibu wa Spika wa Bunge, Job Ndugai.
Kati ya risasi hizo, tano zilimpata katika sehemu mbalimbali za mwili na kusababisha alazwe hospitali tangu wakati huo na kufanyiwa operesheni 17, kwa mujibu wa Chadema.
Katika taarifa yake ya jana aliyoiweka kwenye mitandao ya kijamii, Lissu alisema polisi wameshindwa kumhoji kutokana na kasoro za kiufundi.
"Hadi sasa Mwanasheria Mkuu wa Tanzania hajamwomba Mwanasheria Mkuu mwenzake wa Kenya ruhusa ya mimi kuhojiwa na Polisi wa Kenya juu ya shambulio hilo kama inavyotakiwa na sheria husika za nchi yetu," aliandika Lissu ambaye ni mwanasheria kwa taaluma.
Alipoulizwa maoni yake juu ya kauli hiyo ya Lissu kuwa polisi hawawezi kumuhoji nje ya mipaka ya nchi, IGP Sirro aliiambia gazeti la Nipashe “Mimi sina jibu.”
Wiki iliyopita, IGP Sirro alisema ametuma wapelelezi Nairobi baada ya kusikia Lissu amekubali kuhojiwa juu ya tukio hilo na matarajio yao pia ni kuwapata dereva na mlinzi wake.
“Tumetuma watu wetu kwenda kuchukua maelezo yake (Lissu)," alisema IGP Sirro. "Mwanzo tuliomba kwenda lakini chama (Chadema) walikataa. Juzi tumesikia wamesema wapo tayari".
"Tumetuma vijana wetu wawili kwenda Nairobi kuchukua maelezo yake.”
Alisema lengo kubwa ni kujua mazingira ya shambulio yalikuwaje na kwamba ikiwezekana wampate dereva na msaidizi huyo wa Lissu ili kurahisisha upepelezi wa tukio lenyewe.
“Upelelezi unaingia vitu vingi sana (sasa) kutompata dereva na mlinzi wake Lissu inashindwa kutupa picha kamili ya tukio,” alibainisha.
“Niwaambie Watanzania watuamini, hatuko kwa ajili ya kuona hatumtendei mtu haki, tupo kwa ajili ya kutenda haki.”
Post A Comment: