
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM, Hamphrey Polepole amesema kuwa chama hicho hakina taarifa yoyote ya kurudi kwa Wema Sepetu.
Akijibu swali kuhusu taarifa kuwa Wema amerudi CCM akitokea Chadema, Polepole amesema CCM ina utaratibu wa mwanachama kujiunga na chama hicho.
"Kupitia utaratibu na muundo wetu wa chama kwenye shina kisha ataandikwa kwenye orodha ya wanachama kwenye tawi ambalo yeye ni mkaazi," amesema
Hapo jana Wema Sepetu alitangaza kurudi CCM baada ya kukaa Chadema kwa muda wa miezi kumi tangu alipohamia.
Katika ukurasa wake wa Instagram, Wema aliandika hivi, βSiwezi kuendelea kuishi kwenye nyumba inayonikosesha amani... Peace of mind is everything for me...natangaza rasmi kuondoka Chadema na kurudi nyumbani.β
Mwigizaji wa filamu ambaye pia ni kada wa CCM, Steve Nyerere alipoulizwa kuhusu msanii mwenzake huyo kurudi CCM alisema ni kweli amefanya hivyo.
Akizungumza na waandishi akiwa ameambatana na mama yake mzazi nyumbani kwao Sinza Jijini Dar es Salaam wakati akihamia Chadema, Wema alisema sababu kubwa ya kuhamia ni ili kupata nafasi ya kupigania demokrasia anayodai kuwa inapotea nchini Tanzania.
Sababu nyingine aliyoieleza Wema ni kutelekezwa na CCM licha ya kujitolea kutoa mchango wake kwa chama hicho wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2015 kiasi cha kuwa hatarini kumwagiwa tindikali visiwani Zanzibar.
Hata hivyo, jana alibadili msimamo wake na kurudi CCM. Akizungumzia kuhama kwa Wema, Meya wa Ubungo, Boniface Jacob ambaye alipokea kadi ya CCM kutoka kwa Wema, alisema walikuwa bado hawajamkabidhi msanii huyo kadi ya Chadema na kuwa walikuwa wanatafuta siku maalum ya kufanya hivyo.
Post A Comment: