
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
STRAIKA wa Yanga, Donaldo Ngoma alitarajiwa kutua nchini jana akitokea kwao Zimbabwe, lakini uongozi wa klabu yake umepanga kumchukulia hatua kali kama atatoa majibu yasiyoridhisha.
Ngoma alipewa ruhusa ya kwenda Zimbabwe kwa mapumziko madogo kutokana na kuwa majeruhi, lakini alikaa huko zaidi ya muda aliopewa bila kutoa taarifa.
Kutokana na hilo, mabosi wake wamepanga atakapofika tu aeleze kilichomfanya achelewe na kama atatoa majibu yasiyoridhisha, atachukuliwa hatua kali.
Afisa Habari wa Yanga, Dismas Ten alisema: "Taarifa ya kurudi kwake ilikuwa jana na atakapofika, atatakiwa aeleze kilichomchelewesha na kama hatakuwa na sababu zisizo na mashiko, itabidi ahadhibiwe. Amepewa muda wa kujieleza kwa sababu yeye ni binadam, huenda alikuwa na sababu zenye mashiko.β
Ngoma alipata majeruhi ya msuli wa paja katika mchezo wao na Mtibwa Sugar jijini Dar es Salaam, maumivu
hayoyaliyomweka nje ya uwanja akakosa mechi nne za ligi ikiwemo ya watani wao Simba.
Hata hivyo, inadaiwa mchezaji huyo yuko mbioni kujiunga na Singida United inayofundishwa na kocha wake wa zamani, Mholanzi Hans Pluijm.
Post A Comment: