
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
Ofisa Mtendaji Mkuu na Ofisa Mkuu wa Fedha wa Kampuni ya Acacia, wametangaza kujiuzulu kuanzia jana Novemba 2, 2017.
Kupitia barua yake, Ofisa Mtendaji Mkuu, Brad Gordon amesema anataka kurudi nyumbani kwao Australia kusimamia masuala ya familia yake wakati kwa upande Ofisa Mkuu wa Fedha, Andrew Wray akisema amepata fursa nzuri zaidi.
Pamoja na hatua hiyo.. taarifa hiyo imesema kuwa bado wataendela kuwa chini ya kampuni hiyo mpaka mwisho wa mwaka huu.
Tayari Bodi ya Acacia imewataja Peter Geleta ambaye atakuwa Mkurugenzi Mkuu na Jaco Maritz atakachukua nafasi ya Andrew Wray aliyekuwa Mkurugenzi wa fedha.
Wote wawili walioteuliwa walikuwa watendaji wa Acacia kwa muda mrefu ambapo Geleta alikuwa mkuu wa oganaizesheni wakati Maritz alikuwa meneja mkuu wa idara ya fedha.
Kwa miezi miwili iliyobaki, makabidhiano ya ofisi yataendelea kufanyika mpaka Januari Mosi, mwakani yatakapohitimishwa na uongozi mpya kuendelea kutekeleza majukumu yake.
Post A Comment: