
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi 🇵🇪🇵🇪
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
ALIYEKUA Rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe, amekataa kuishi uhamishoni akisema atafia nchini mwake, jambo lililofanya jeshi kumpa kinga ya kutoshtakiwa yeye na mkewe na pia amepewa stahili zote anazopaswa kupata kama mstaafu.
Awali ilielezwa kuwa Mugabe alikuwa anaombwa akaishi uhamishoni Zambia, jambo ambalo mkongwe huyo wa siasa za Afrika alilikataa.
Shirika la Habari la Reuter, jana liliripoti kuwa Mugabe alisisitiza kutoondoka nchini humo, badala yake apewe ulinzi wa kutosha yeye na familia yake na kinga ya kutoshtakiwa.
Chanzo cha habari cha Serikali kilichokuwa katika meza ya majadiliano, kilisema Mugabe alisema kwamba alitaka kufia Zimbabwe na hana mpango wa kuishi ugenini.
Kikizungumza hilo kwa hisia na kusisitiza, chanzo hicho ambacho hakikuwa tayari kutajwa kwa vile hakina mamlaka ya kufanya hivyo kilisema kuwa kwake ni muhimu sana kupatiwa usalama wa kuishi nchini, ijapokuwa hilo halitamzuia kusafiri ng’ambo akitaka au ikibidi.
“Mugabe anafahamu kuwa umma unamchukia mkewe na wengi wana hasira namna anavyoendesha maisha ya anasa pamoja na kuingilia siasa za ZANU-PF.
Katika hali hiyo, ilikuwa lazima kumhakikishia yeye na mkewe pia usalama,” chanzo kingine kilisema.
JESHI LATHIBITISHA KINGA
Jana jioni, Jeshi la Zimbabwe (ZDF), lilithibitisha kuwa Mugabe na mkewe wamepewa kinga ya kutoshtakiwa, na wameruhusiwa kuishi chini humo.
Msemaji wa ZDF, Kanali Overson Mugwisi, aliliambia Shirika la Habari la Marekani (CNN), kuwa makubaliano yamefikiwa na Mugabe, ikiwamo kinga ya kutoshtakiwa na kuhakikishiwa usalama wake na mkewe Grace.
Mugabe alitumia wiki nzima kujadili kuondoka kwake kwa amani baada ya shinikizo la chama chake na jeshi lililotwaa madaraka na kumweka kizuzini.
Katika majadiliano marefu ambayo awali maofisa wa jeshi walikuwa tayari kumsamehe Mugabe lakini si mkewe, majenerali walilazimika kwa shingo upande kumkubalia masharti yake, ikiwamo kutogusa mali zake zinazodaiwa kupatikana isivyo halali.
Baada ya kutangazwa kwa kinga hiyo, Mugabe atapatiwa marupurupu ya kustaafu, ikiwamo pensheni, makazi, posho ya likizo na usafiri, bima ya afya, usafiri wa ndege na usalama.
Chanzo kingine cha habari kilicho karibu na familia yake, kimesema kutokana na kuathirika kisaikolojia kulikotokana na mlolongo wa mambo uliomtokea kipindi cha wiki moja hadi kufikia kujiuzulu, Mugabe anatarajia kusafiri kwenda Singapore kwa uchunguzi wa afya yake wiki chache zijazo.
“Alikuwa asafiri Singapore katikati ya Novemba mwaka huu kabla ya jeshi kumweka katika kizuizi cha nyumbani,” kilisema chanzo hicho.
Mugabe amekuwa akisisitiza kuwa yeye na familia yake wanaishi maisha ya kawaida na hamiliki utajiri wowote nje ya Zimbabwe.
Lakini mgogoro baina ya Grace na mfanyabiashara mmoja wa Ubelgiji kuhusu pete ya dhahabu yenye thamani ya dola milioni 1.3, ulianika staili ya maisha ya anasa ya Mugabe na mkewe aliyepachikwa jina la “Gucci Grace” kwa sifa yake ya kufanya manunuzi ya bei mbaya.
Post A Comment: