
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
Aliyekuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Frederick Sumaye ambaye kwa sasa ni mwanachama wa CHADEMA, amesema upinzani hauwezi kukubali kuacha CCM iendelee wakati hali ya maisha ya watu inaendelea kuwa mbaya.
Sumaye ameyasema hayo alipokuwa akiongea kwenye mkutano Kimara jijini Dar es salaam alipokuwa akimnadi mgombea udiwani wa CHADEMA, na kusema kwamba hali ya uchumi na maisha ya wananchi kwa sasa ni mbaya zaidi, lakini iwapo wakisema ukweli wanaonekana ni waongo hivyo sio suala la kuendelea kulifumbia macho na kuacha CCM iendelee kutawala.
"Hatuwezi kukubali CCM iendelee kutawala nchi hii wakati watu wanazidi kuwa na hali mbaya ya maisha, tukiwaambia watu wana hali mbaya wanasema tunasema uongo, tukisema uchumi umezama wanasema tunasema uongo, kama tunasema uongo kwa nini hali za wananchi zinakuwa mbaya, maana kuna vitu ambavyo havijifichi, kama uchumi unakwenda vizuri tafsiri zake itaionekana kwenye hali ya wananchi, hali ya wananchi ni mbaya", amesema Sumaye.
Hivi karibuni kumekuwa na mvutano kati ya vyama vya upinzani kudai kuwa uchumi wa nchi umeshuka, huku serikali ikikanusha na kuoa taarifa kuwa suala hilo halina ukweli wowote, kwani uchumi wa nchi umetengemaa kutokana na kubana matumizi.
Post A Comment: