
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
Mbunge wa Iringa Mjini kwa tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mchungaji Peter Msigwa amefunguka na kuonyesha nia yake ya kutaka kumuondoa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai iko pale pale.
Mchungaji Msigwa mwezi Oktoba 2017 alionyesha nia ya kupeleka hoja Bungeni ili kumuondoa Spika Job Ndugai katika nafasi yake hiyo na kusema atatumia kanuni za Bunge na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kufanya hivyo kwa kile anachoamini kuwa Spika wa Bunge ameshindwa kusimama vyema katika nafasi hiyo jambo ambalo limepelekea Bunge hilo sasa kuonekana halina nguvu na kushindwa kuisimamia serikali.
Msigwa amesema kuwa anaamini kuwa wabunge mbalimbali ambao wana akili wataungana na hoja yake hiyo ya kutaka kumuondoa Spika Job Ndugai katika kiti hicho kwa kutumia kanuni za Bunge na Katiba ya nchi.
"Hoja ya kumungβoa spika iko pale pale! Naamini wabunge Wenye akili wataiunga mkono" aliandika Mbunge Msigwa kupitia mtandao wake wa Instagram
Wabunge mbalimbali wa upinzani wamekuwa wakitoa lawama kuwa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hivi sasa linashindwa kuisimamia serikali ipasavyo na wengine wamekuwa wakidai kuwa Bunge hilo linaendeshwa na serikali, jambo ambalo limemfanya Mbunge Msigwa kutaka kupeleka hoja ya kumuondoa kiongozi wa Bunge hilo Spika Job Ndugai.
Post A Comment: