
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
Mshambuliaji mwenye hasira, Sadio Mane amembwatukia kocha wake, Jurgen Klopp baada ya kumwingiza dakika ya 89, wakati Liverpool ikicheza na Chelsea.
Mane alikosa uvumilivu baada ya kuwekwa benchi kwa dakika 89 katika mchezo wa sare ya bao 1-1kwenye Uwanja wa Anfield.
Klopp alijaribu kumtuliza mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Senegal, ambaye alishindwa kuficha hasira yake na mashabiki waliofurika uwanjani hapo waliona kila kitu.
Kocha huyo wa Ujerumani, Klopp alisema: "Nilimpigia kelele kwa sababu alikuwa katikati ya uwanja wakati mimi nilitaka acheze kama winga wa kulia."
Klopp alikuwa katikati ya mzozo na mchezaji huyo mara tu baada ya kumalizika kwa mchezo huo na kulazimika kumwelewesha alichokuwa anataka kwake.
Bosi huyo wa Liverpool alianza kuwasumbua na kuwabwatukia waamuzi kwa kuchelewasha kufanya mabadiliko ya kumwingiza Adam Lallana.
Lakini licha ya kumalizana na waamuzi, raia huyo wa Ujerumani aliingia tena katika mzozo na Mane mara baada ya kumalizika kwa mchezo huo wakipishana kauli.
Mane alikasirishwa na kitendo cha kuingia dakika moja kabla ya mchezo kumalizika, akishindwa kuficha hasira zake kwa kucheza dakika chache katika mchezo huo mkubwa.
Liverpool walianza kupata bao la kuongoza kupitia kwa mshambuliaji wa kimataifa wa Misri, Mohamed Salah dhidi ya timu yake ya zamani, likiwa bao lake la 15 msimu huu akiwa na Liverpool.
Lakini Willian aliisawazishia Chelsea zikiwa zimebaki dakika tano mchezo kumalizika, baada ya kumwinulia mpira kipa Simon Mignolet, dakika chache kabla ya mwamuzi Michael Oliver kumzuia Lallana asiingie uwanjani.
Post A Comment: