
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
Kiungo wa Singida United, Deus Kaseke, amekiri mchezo ujao dhidi ya Yanga utakuwa wa aina yake kutokana na kuzikutanisha timu zenye wachezaji bora.
Singida United itaikaribisha Yanga Jumamosi katika mchezo utakofanyika Uwanja wa Namfua, Singida ambao utatumika kwa mara ya kwanza baada ya kufanyiwa ukarabati.
Kaseke, ambaye msimu uliopita aliitumikia Yanga, alisema atakuwa na kibarua kigumu kukutana na timu yake ya zamani katika mchezo huo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
Alisema mkakati wa Singida United ni kupanda katika nafasi za juu kwenye msimamo wa ligi, hivyo lazima wapambane kuhakikisha wanashinda mchezo huo baada ya kutoka suluhu juzi na Mtibwa Sugar ugenini.
"Nawaheshimu Yanga ni timu nzuri ina wachezaji wenye ubora kama Singida United, itakuwa mechi bora," alisema mshambuliaji huyo wa pembeni.
Kaseke alisema kutoka suluhu na Mtibwa Sugar walirejea nyumbani Singida kujipanga kwa mchezo huo aliodai ni muhimu kupata pointi tatu.
Mchezo huo utakuwa wa pili kwa timu hizo kupepetana mwaka huu na katika mechi ya kirafiki Singida United ililala mabao 3-2.
Mchezo huo unatarajia kuwa na mvuto wa aina yake kwa kuwa Singida ina wachezaji kadhaa waliowahi kuwika Yanga kipa Ali Mustapha 'Barthez', Nizar Khalfan, Kigi Makassi, Atipele Green na Kaseke.
Singida United inanolewa na kocha wa zamani wa Yanga Mdachi Hans Van Der Pluim, aliyekuwa kipenzi cha mashabiki wa klabu hiyo ya Jangwani.
Post A Comment: