
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi 🇵🇪🇵🇪
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
WACHEZAJI wawili muhimu ndani ya kikosi cha Simba, Emmanuel Okwi na Jjuuko Murushid, ambao waliukosa mchezo uliopita dhidi ya Prisons, kutokana na kuwa nchini kwao Uganda, sasa wamerejea na wapo tayari kwa mapambano.
Wawili hao walikuwa kwenye kikosi cha timu yao ya Taifa ya Uganda, ‘The Crane,’ huku Okwi akidai kuwa na majeraha, lakini sasa wamewasili tayari kuwawinda Lipuli FC, mchezo unaotarajiwa kuchezwa mwishoni mwa wiki hii kwenye Uwanja wa Chamazi, jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na gazeti la DIMBA Jumatano jana, Meneja wa timu hiyo, Richard Robert, alithibitisha kuwa, wachezaji hao wapo nchini na kwamba wapo tayari kwa mapambano, hasa mchezo dhidi ya Lipuli.
“Tunashukuru kwamba wachezaji wetu hao wameshawasili na wapo tayari kwa mapambano, Okwi alikuwa majeruhi, lakini imeonekana hayakuwa makubwa, lakini Jjuuko yeye yupo fiti kabisa,” alisema.
Richard alisema kikosi cha timu yao kipo vizuri na wanachokisubiri ni siku hiyo ya kuwakabili Lipuli, kwani malengo yao ni kuhakikisha kila mchezo wanaibuka na ushindi mpaka watakapotwaa ubingwa.
Simba wataingia katika mchezo huo wakiwa na ari baada ya kutoka kuzifunga timu za Mbeya, yaani Mbeya City waliowafunga bao 1-0, wakapata tena ushindi kama huo dhidi ya Tanzania Prisons.
Post A Comment: