
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
NAHODHA wa Prisons, Laurian Mpalile, amefichua siri ya kufungwa bao 1-0 na Simba katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, uliochezwa kwenye Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya wiki iliyopita.
Akizungumza na gazeti la BINGWA , Mpalile alisema alijua mshambuliaji wa Simba, John Bocco, angewafunga katika mchezo huo.
Mpalile alisema Bocco hakubahatisha kuwafunga, kwani amekuwa akiwafunga mara nyingi kila wanapokutana.
Alisema Bocco ni mchezaji anayewasumbua kwa muda mrefu tangu akiwa anaitumikia Azam FC alikuwa anawafunga nyumbani na ugenini.
Mpalile alisema wamekuwa wakijitahidi kumdhibiti mshambuliaji huyo, lakini ni mara chache wanafanikiwa kumzuia.
Alisema walijua mapema Bocco angewafunga na ndicho kilichotokea katika mchezo wao wa Jumamosi iliyopita.
βSijui tuseme Bocco ana bahati ya kutufunga au vipi kwa sababu kila tunapokutana naye kwenye mechi lazima atufunge, ametufunga zaidi ya mara tatu, Chamazi na Sokoine,β alisema Mpalile.
Alisema katika mchezo wa marudiano itabidi wajipange ili makosa yasirudie na baadaye kuondoka na ushindi.
Simba kwa sasa wanaongoza katika msimamo wa ligi hiyo kutokana na pointi 22 sawa na Azam, lakini wakitofautiana mabao ya kufunga na kufungwa.
Post A Comment: