
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi 🇵🇪🇵🇪
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
SERIKALI imeunda timu maalumu ya wataalamu 11 kwa ajili ya kuchunguza ubora wa vichwa 13 vya treni vilivyotelekezwa katika bandari ya Dar es Salaam.
Wakati timu hiyo ikiundwa, serikali imesema itavinunua vichwa hivyo endapo vitabainika kuwa katika ubora.
“Tukishajiridhisha kwenye ubora wa vichwa vile tutakaa na walioleta vichwa na kuanza kuzungumza kwani nia ya serikali ni kufanyakazi na wadau mbalimbali.
Tukishajiridhisha kama vichwa vile vipo katika ubora unaotakiwa baadaye tuweze kuvinunua na kuanza kutumika,” alisema jana Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarwa, alipofanya ziara bandarini kukagua ujenzi wa mashine za ukaguzi (scanner).
“Kama mnavyojua tunajenga miundombinu mingi hapa kwenye bandari yetu na bila kuwa na treni iliyo imara na vichwa vilivyo imara na vya kutosha hatutaweza kuhudumia mizigo yote inayopita katika bandari yetu ya Dar es Salaam.”
Alisema kwa kutambua jambo hilo, serikali imeona kuna haja ya kufanya tathimini ya vichwa hivyo na kwamba kuna wataalamu wazuri wa kukagua ili kupata ubora wake.
Alisema timu hiyo itamaliza kazi yake ndani ya siku 10 zijazo na kwamba tangu waanze tathimini hiyo wana siku nne.
Julai, mwaka huu, Rais John Magufuli alipofika bandarini hapo kwa ajili ya uwekaji wa jiwe la msingi upanuzi wa bandari ya Dar es Salaam, aliagiza apatiwe maelezo kuhusiana na vichwa hivyo pamoja na mmiliki wake.
Rais Magufuli alisema kuwa ana taarifa ya uwepo wa vichwa 13 vya treni bandarini hapo ambavyo mmiliki wake hajulikani na kwamba inaelezwa kuwa ni vibovu.
Hata hivyo, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Deusdedit Kakoko, alisema vichwa hivyo vina nembo ya TRL (Kampuni ya Reli Tanzania) na kwamba ulitokea mgogoro kati ya TRL na kampuni iliyotengeneza baada ya kubainika kuwa mchakato mzima wa manunuzi haukuwa sahihi.
TRL ilinunua vichwa 15 vya treni kutoka kampuni ya EMD (Electro-Motive Diesel)ya Marekani na utengenezaji wake ukafanywa na Kampuni ya DCD ya Afrika Kusini.
Kuhusu ujenzi wa mashine za scanner, Profesa Mbarawa alisema unatarajia kukamilika mwezi ujao na kwamba utaimarisha ulinzi zaidi bandarini na kusimamia mapato kikamilifu.
Ujenzi wa mashine hizo mbili ambazo umegharimu Sh. bilioni 27 na kwamba mashine hizo ni muhimu kwa usalama wa bandari na zitasaidia kuimarisha ulinzi. pia alisema ni za kisasa na zina uwezo mkubwa wa kutambua vitu vya aina mbalimbali ambavyo vitapita bandarini hapo.
“Tukishajiridhisha kwenye ubora wa vichwa vile tutakaa na walioleta vichwa na kuanza kuzungumza kwani nia ya serikali ni kufanyakazi na wadau mbalimbali.
Tukishajiridhisha kama vichwa vile vipo katika ubora unaotakiwa baadaye tuweze kuvinunua na kuanza kutumika,” alisema jana Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarwa, alipofanya ziara bandarini kukagua ujenzi wa mashine za ukaguzi (scanner).
“Kama mnavyojua tunajenga miundombinu mingi hapa kwenye bandari yetu na bila kuwa na treni iliyo imara na vichwa vilivyo imara na vya kutosha hatutaweza kuhudumia mizigo yote inayopita katika bandari yetu ya Dar es Salaam.”
Alisema kwa kutambua jambo hilo, serikali imeona kuna haja ya kufanya tathimini ya vichwa hivyo na kwamba kuna wataalamu wazuri wa kukagua ili kupata ubora wake.
Alisema timu hiyo itamaliza kazi yake ndani ya siku 10 zijazo na kwamba tangu waanze tathimini hiyo wana siku nne.
Julai, mwaka huu, Rais John Magufuli alipofika bandarini hapo kwa ajili ya uwekaji wa jiwe la msingi upanuzi wa bandari ya Dar es Salaam, aliagiza apatiwe maelezo kuhusiana na vichwa hivyo pamoja na mmiliki wake.
Rais Magufuli alisema kuwa ana taarifa ya uwepo wa vichwa 13 vya treni bandarini hapo ambavyo mmiliki wake hajulikani na kwamba inaelezwa kuwa ni vibovu.
Hata hivyo, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Deusdedit Kakoko, alisema vichwa hivyo vina nembo ya TRL (Kampuni ya Reli Tanzania) na kwamba ulitokea mgogoro kati ya TRL na kampuni iliyotengeneza baada ya kubainika kuwa mchakato mzima wa manunuzi haukuwa sahihi.
TRL ilinunua vichwa 15 vya treni kutoka kampuni ya EMD (Electro-Motive Diesel)ya Marekani na utengenezaji wake ukafanywa na Kampuni ya DCD ya Afrika Kusini.
Kuhusu ujenzi wa mashine za scanner, Profesa Mbarawa alisema unatarajia kukamilika mwezi ujao na kwamba utaimarisha ulinzi zaidi bandarini na kusimamia mapato kikamilifu.
Ujenzi wa mashine hizo mbili ambazo umegharimu Sh. bilioni 27 na kwamba mashine hizo ni muhimu kwa usalama wa bandari na zitasaidia kuimarisha ulinzi. pia alisema ni za kisasa na zina uwezo mkubwa wa kutambua vitu vya aina mbalimbali ambavyo vitapita bandarini hapo.
Post A Comment: