
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi 🇵🇪🇵🇪
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
SHEIKH Issa Ponda amepewa siku tatu na Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa, awe amejisalimisha kwa chombo hicho cha dola kwa madai ya kufanya uchochezi juzi.
Katika mkutano wake na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam juzi, Sheikh Ponda ambaye pia ni Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislam Tanzania, anadaiwa kutoa kauli za kichochezi na zisizofaa katika jamii.
Kamanda Mambosasa alisema jijini jana kuwa kitendo cha Sheikh Ponda kulikimbia Jeshi la Polisi baada ya mkutano huo hakitamsaidia na kwamba ni heri ajisalimishe, "ili awe sehemu salama".
Alisema jeshi hilo halikufanikiwa kumnasa wakati wa mkutano wake huo na waandishi wa habari kwa kuwa halikupata taarifa sahihi kuhusu mkutano huo na muda wa kufanyika kwake.
"(Waandishi) wengine mliambiwa mkutano huu ungefanyika saa nne asubuhi, lakini ulianza mapema hivyo tulimkosa kidogo tu kumkamata," alisema Mambosasa. "Akijisalimisha kabla ya siku hizi tatu itakuwa ni salama zaidi."
Katika mkutano wake wa juzi uliofanyika Kariakoo jijini, Sheikh Ponda alieleza ziara yake ya jijini Nairobi kumjulia hali Mbunge wa
Singida Mashariki, Tundu Lissu (Chadema) na mikakati ya mtaalamu huyo wa sheria kurejea katika siasa baada ya kupona.
Kamanda Mambosasa alisema jijini jana kuwa kitendo cha Sheikh Ponda kulikimbia Jeshi la Polisi baada ya mkutano huo hakitamsaidia na kwamba ni heri ajisalimishe, "ili awe sehemu salama".
Alisema jeshi hilo halikufanikiwa kumnasa wakati wa mkutano wake huo na waandishi wa habari kwa kuwa halikupata taarifa sahihi kuhusu mkutano huo na muda wa kufanyika kwake.
"(Waandishi) wengine mliambiwa mkutano huu ungefanyika saa nne asubuhi, lakini ulianza mapema hivyo tulimkosa kidogo tu kumkamata," alisema Mambosasa. "Akijisalimisha kabla ya siku hizi tatu itakuwa ni salama zaidi."
Katika mkutano wake wa juzi uliofanyika Kariakoo jijini, Sheikh Ponda alieleza ziara yake ya jijini Nairobi kumjulia hali Mbunge wa
Singida Mashariki, Tundu Lissu (Chadema) na mikakati ya mtaalamu huyo wa sheria kurejea katika siasa baada ya kupona.
Pia alizungumzia hali ya usalama na siasa nchini.
Post A Comment: