Mesut Ozil amewajibu wadau wanaoponda kiwango chake akidai amekuwa akicheza kwa nguvu zote na mepenzi makubwa Arsenal.


Kauli ya Mjerumani huyo imekuja, baada ya wadau kukosoa uchezaji wake wakidai hana msaada Emirates licha ya kununuliwa kwa bei mbaya kutoka Real Madrid kwa Pauni 42 milioni akiwa ndiye mchezaji ghali zaidi kununuliwa na klabu hiyo.

"Siku zote nimekuwa nikijitahidi kuifanyia mambo makubwa Arsenal, lakini sina furaha katika nafasi ya uwanjani ninayopangwa,"alisema Ozil mwenye miaka 29.

Mchezaji huyo amekuwa akihusishwa na mpango wa kumfuata bosi wake wa zamani Jose Mourinho kujiunga na Manchester United katika dirisha dogo Januari, mwakani.

Mkataba wake unatarajia kumalizika mwishoni mwa msimu huu na Arsenal imemuweka sokoni ikitaka kumpiga bei mapema ili kupata fedha.
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: