
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa Chadema katika kata ya Bomani wilayani Tarime, Morice Matius amehamia CCM akidai kuvutiwa na mabadiliko ya chama hicho.
Akikabidhi kadi ya Chadema, skafu mbili na fulana mbili za chama hicho kwenye mkutano wa halmashauri ya CCM wilayani hapa, Matius ambaye pia ni mjumbe wa Serikali ya mtaa wa Buhemba alisema ameamua kujiunga na chama hicho kutokana na mabadiliko yanayofanywa na Serikali.
Alisema moja ya ajenda iliyokuwa ikizungumzwa na Chadema kipindi cha nyuma ni kutokuwapo kwa ndege za Serikali, mikataba mibovu ya madini na kero zingine ambazo zimeanza kutatuliwa huku nyingi zikiwa zinapatiwa ufumbuzi.
Mkuu wa wilaya ya Tarime, Glorius Luoga alisema kila mwanachama wa CCM anatakiwa kwenda na kasi ya Serikali iliyopo madarakani.
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) Wilaya ya Tarime, Godfrey Frances alisema moja ya sababu ya upinzani kushinda kwenye chaguzi ni kutokana na baadhi ya viongozi wa CCM kutokuwa tayari katika kutetea masilahi ya wananchi.
Post A Comment: