
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Freeman Mbowe ameitaka serikali kubadili uamuzi wa kuzuia mikutano na shughuli nyingine za siasa kwa kuwa Tanzania ilishakubali na kuingia katika mfumo wa vyama vingi vya siasa kwa mujibu wa sheria.
Akizungumza na wananchi kwenye mkutano wake wa kumnadi mgombea wa Udiwani katika Kata ya Kitwiru Manispaa ya Iringa, Mbowe amesema serikali iliyopo madarakani imechaguliwa kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano hivyo inapaswa kuheshimu sheria pamoja na katiba hiyo ikiwemo sheria namba 5 iliyorejesha mfumo huo mwaka 1992 kabla ya hapo awali kufutwa mwaka 1965.
Kwa upande wa Mbunge wa Iringa Mjini Mchungaji Peter Msigwa amewataka wananchi wa Kata ya Kitwiru kuchagua mgombea wa Chadema ili aongeze nguvu kwenye baraza la madiwani linaloongozwa na chama hicho ambalo limeifanya Manispaa ya Iringa kuwa mfano wa kuigwa katika uendeshaji halmashauri nchini.
Naye Mgombea wa Udiwani kupitia chama hicho, Bahati Chengula amewataka wananchi kuendelea kumwamini kama walivyomwamini awali na kumchagua kuwa Mwenyekiti wa mtaa, kazi ambayo ameifanya kwa uadilifu na kujituma kwa lengo la kusukuma mbele maendeleo yao.
Post A Comment: