WAZIRI Mkuu mstaafu, Edward Lowassa, amehudhuria kampeni za uchaguzi mdogo wa udiwani Kata ya Muriet mkoani Arusha huku akitaka upinzani kuchukua nchi mwaka 2020.


“Nimekuja kumnadi mgombea udiwani wa Kata ya Muriet, Simon Moses Mollel, (Chadema) mpeni kura nyingi za ushindi,” alisema.

Kauli hiyo ameitoa katika mkutano wa kampeni za uchaguzi wa udiwani wa Kata ya Muriet, uliofanyika eneo la sokoni kwa Mrombo jijini Arusha.

“Nawashukuruni mwaka 2015, mlinipa kura nyingi zaidi ya milioni sita, Watanzania mlinipa kura nyingi sana mpaka mkanitungia jina la Rais wa mioyo ya watu,”..........Nasema watusubirie mwaka 2020 tutawaonyesha kazi, lazima tuchukue nchi mapema.”
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: