
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
Miongoni mwa madiwani waliojiuzulu wakiwa Chadema kwa kile walichosema ni kumuunga mkono Rais John Magufuli, wameanguka kwenye kura ya maoni ya CCM ngazi ya kata.
Kuanguka kwa madiwani hao ni kinyume cha ahadi ya Rais Magufuli aliyoitoa akiwa mkoani Arusha ambako alipendekeza madiwani hao wapewe kipaumbele ndani ya CCM.
Rais Magufuli pia alipendekeza madiwani hao wapewe kipaumbele cha kupitishwa kugombea udiwani kupitia CCM katika uchaguzi mdogo unaotarajiwa kufanyika Novemba 26 ukihusisha kata 43 nchini.
Katibu wa Uenezi wa CCM Mkoa wa Arusha, Shaaban Mdoe amesema kuanguka kwa madiwani si hoja kwa sababu hiyo ni ngazi ya kata na bado mchakato wa uchaguzi unaendelea.
Mdoe amesema baada ya kura ya maoni ndani ya kata, majina yatapelekwa katika Sekretarieti ya Wilaya kwa ajili ya mchujo na baadaye ngazi ya mkoa ili kupendekeza jina la mgombea, kazi itakayokamilika kabla ya Oktoba 20 mwaka huu.
Walioangushwa katika kura ya maoni ni Anderson Sikawa aliyekuwa diwani wa Leguruki, Greyson Isangya (Maroroni), Josephine Mshiu (Viti Maalumu), Emmanuel Mollel (Makiba) na Japhet Jackson (Embuleni).
Post A Comment: