
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi 🇵🇪🇵🇪
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
IKIWA imebakia siku moja kabla ya mchezo wa watani wa jadi, Kocha wa Yanga, George Lwandamina, amesema kwake ni pigo kuwakosa nyota wake wa kimataifa, Amis Tambwe, Donald Ngoma na Thaban Kamusoko kwenye mchezo huo wa kesho.
Yanga ambayo inarejea leo jijini Dar es Salaam ikitokea Morogoro ilipoweka kambi kujiandaa na mchezo wa kesho dhidi ya Simba, itakosa huduma ya wachezaji hao ambao walibaki Dar es salaam kujiuguza majeraha yao.
Akizungumza na gazeti la Nipashe, Lwandamina, alisema kuwa kukosa huduma ya nyota hao kwenye mchezo mkubwa na wenye upinzani kama wa kesho ni changamoto kwake.
“Nashukuru wachezaji wangu wapo katika ari nzuri, lakini kama mnavyojua Tambwe, Ngoma na Kamusoko hatupo nao huku (Morogoro) wapo Dar es Salaam wakiendelea kujiuguza, nilitamani sana kuwa nao kwenye mchezo wa Jumamosi kwa sababu ni wachezaji wenye uzoefu,” alisema Lwandamina.
Alisema kuwa pamoja na kuwakosa nyota hao, hiyo haiwezi kuwa sababu ya kupoteza mchezo huo na wamejipanga kupambana ili kupata pointi tatu.
“Naamini wachezaji ambao ninao wanaweza wakaifanya kazi nzuri Jumamosi..., tunaye Ajibu (Ibrahimu) na Chirwa (Obbrey) kwenye safu ya ushambuliaji ambao wamekuwa wakifanya vizuri,” alisema Lwandamina.
Aidha, Meneja wa timu hiyo, Hafidh Saleh, aliiambia gazeti la Nipashe jana kuwa kikosi cha timu hiyo kinarejea Dar es Salaam leo mara baada ya mazoezi ya asubuhi tayari kuwakabili vinara hao wa ligi kuu.
“Hatuna majeruhi miongoni mwa wachezaji tulionao huku (Morogoro) na tunaomba wachezaji wandelee kuwa katika ari nzuri, tunarejea kesho (leo)asubuhi tutaingia kambini mpaka siku ya mchezo,” alisema Saleh.
Mchezo huo unatazamiwa kuwa na upinzani mkubwa hasa kutokana na ubora wa vikosi vya timu hiyo waliouonyesha kwenye michezo miwili iliyopita.
Akizungumza na gazeti la Nipashe, Lwandamina, alisema kuwa kukosa huduma ya nyota hao kwenye mchezo mkubwa na wenye upinzani kama wa kesho ni changamoto kwake.
“Nashukuru wachezaji wangu wapo katika ari nzuri, lakini kama mnavyojua Tambwe, Ngoma na Kamusoko hatupo nao huku (Morogoro) wapo Dar es Salaam wakiendelea kujiuguza, nilitamani sana kuwa nao kwenye mchezo wa Jumamosi kwa sababu ni wachezaji wenye uzoefu,” alisema Lwandamina.
Alisema kuwa pamoja na kuwakosa nyota hao, hiyo haiwezi kuwa sababu ya kupoteza mchezo huo na wamejipanga kupambana ili kupata pointi tatu.
“Naamini wachezaji ambao ninao wanaweza wakaifanya kazi nzuri Jumamosi..., tunaye Ajibu (Ibrahimu) na Chirwa (Obbrey) kwenye safu ya ushambuliaji ambao wamekuwa wakifanya vizuri,” alisema Lwandamina.
Aidha, Meneja wa timu hiyo, Hafidh Saleh, aliiambia gazeti la Nipashe jana kuwa kikosi cha timu hiyo kinarejea Dar es Salaam leo mara baada ya mazoezi ya asubuhi tayari kuwakabili vinara hao wa ligi kuu.
“Hatuna majeruhi miongoni mwa wachezaji tulionao huku (Morogoro) na tunaomba wachezaji wandelee kuwa katika ari nzuri, tunarejea kesho (leo)asubuhi tutaingia kambini mpaka siku ya mchezo,” alisema Saleh.
Mchezo huo unatazamiwa kuwa na upinzani mkubwa hasa kutokana na ubora wa vikosi vya timu hiyo waliouonyesha kwenye michezo miwili iliyopita.
Post A Comment: