
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
Mechi mbili za kuamua hatma ya washambuliaji Mrundi Laudit Mavugo na Mghana Nicholas Gyan katika kikosi cha Simba.
Mmoja kati ya washambuliaji hao wawili atafungasha virago kumpisha Mnigeria Mussalawal Ibrahim kuingia katika kikosi cha Simba wakati wa kufunguliwa kwa dirisha dogo la usajili Novemba 15.
Simba kwa sasa inaendelea na maandalizi yake ya kujindaa na mechi yake dhidi ya Mbeya City kwenye Uwanja wa Sokoine na wiki moja baadae watacheza tena na Tanzania Prison katika uwanja huo.
Simba baada ya kucheza mechi dhidi ya Prison dirisha dogo la usajili litafunguliwa na huenda kuna moja ya mchezaji wa kigeni kuachwa na kiingizwa jina la Mnigeria Ibrahim.
Ibrahim amejiunga na Simba na kufanya mazoezi nayo tangu akiwa Zanzibar kama kocha Joseph Omog atalizika na kiwango chake basi lazima kumuondoa mchezaji mmoja wa kigeni.
Bila shaka kati ya Mrundi Mavugo na Mghana Gyan mmoja wao ataachwa ili kumpisha Ibrahim.
Mkataba wa Mavugo unamalizika mwisho wa msimu huu na ameshindwa kabisa kufikia ubora wake wa msimu uliopita kwani hadi sasa ameshafunga mabao mawili tu.
Gyan alisajiliwa na Simba kwa mbwembwe akitokea nchini Ghana katika klabu Ebusua Dwarfs akiwa mfungaji bora, lakini tangu alipotua nchini ameshindwa kabisa kuonyesha makali yake.
Bila shaka nafasi ya Ibrahim ipo wazi, lakini kama ataweza kumlizisha kocha Omog na msaidizi wake Masoud Djuma katika mazoezi ambayo anaendelea kufanya na kikosi hiko tangu alipojiunga wakiwa Zanzibar.
Post A Comment: