
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) limewataja askari wawili waliouawa na kundi la wapiganaji la ADF wakati wakilinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).
Askari hao wametajwa kuwa ni Koplo Maselino Paschal Fubusi na Praiveti Venance Moses Chimboni.
Imeelezwa askari wengine 12 wamejeruhiwa katika shambulio lililofanywa na kundi hilo.
Taarifa ya Kurugenzi ya Habari na Uhusiano ya JWTZ iliyotolewa jana Jumanne imesema, βAskari hao wamefariki baada ya kushambuliwa kwa kupigwa risasi na kundi la waasi, tukio lililotokea Oktoba 9 umbali wa kilomita 24 mashariki mwa mji wa Beni.β
Amesema, βMajeshi yetu yamewarudisha nyuma waasi hao na kudhibiti eneo. Kutokana na shambulio hilo, Umoja wa Mataifa umeunda bodi ya uchunguzi wa tukio hilo,β imesema taarifa hiyo.
Imeelezwa maofisa na askari wa JWTZ wanaendelea kutekeleza majukumu yao katika operesheni hiyo.
Kuhusu miili ya askari hao kurejeshwa nchini, taarifa imesema Umoja wa Mataifa unaandaa utaratibu na itakapokamilisha wataujulisha umma mapokezi, kuaga na mazishi yatakavyokuwa.
Post A Comment: