
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
RAIS John Magufuli amewatumia salamu wakurugenzi wote ambao ni walevi na kuwataka kuacha mara moja kabla ya kufukuzwa kazi.
Rais Magufuli alituma salamu hizo jana alipokuwa akifungua Mkutano Mkuu wa 33 wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa (ALAT) jijini Dar es Salam.
Alisema amepata taarifa kwamba kuna baadhi ya wakurugenzi katika halmashauri ambao ni walevi na kwamba endapo hawatabadilika watafukuzwa kazi.
βNimepata taarifa za watu watatu wanne hivi wakurugenzi ambao ni walevi sana. Kama uko mkurugenzi hapa na ni mlevi ni bora uache kabisa tabia za ulevi, maana tukiwagundua tutawafukuza,β alisema Rais Magufuli na kuongeza:
βNi lazima tujenge maadili ya nchi hatuwezi kukubali kuacha tabia hizi ziendelee.β
Pia Rais Magufuli Alisema kumekuwapo na mgawanyiko wa makundi kwa watumishi katika halmashauri hizo jambo linalochangia kupunguza ufanisi mzuri wa kazi, hivyo kuagiza halmashauri kumaliza makundi hayo.
βSisi sote tunajenga nyumba moja, lakini kwenye halmashauri kuna makundi. Unaweza kukuta kundi hili la watumishi liko upande wa wakurugenzi, lingine kwa Meya, au la chama fulani. Nawaomba muondoe makundi na migogoro ili mfanye kazi kwa ufanisi ndio maana nimefurahi leo kuona madiwani wa vyama vingine,β alisema.
Alisema yeye adui ni wale wanaoiibia serikali rasilimali zake, hivyo ni bora nguvu kubwa ikaelekezwa huko kupambana nao.Sambamba na hilo, aliwaomba viongozi katika halmashauri hizo kuhamasisha amani na upendo wa nchi ikiwamo kufanya shughuli za maendeleo na uzalendo hususani ulipaji wa kodi.
Alisema hakuna nchi duniani ambayo iliendelea bila wananchi wake kulipa kodi na kwamba atahakikisha kila fedha inayopatikana inatumika kikamilifu kwa manufaa ya Watanzania wote.
Akitolea mfano wa madini ya Tanzanite yaliyokamatwa hivi karibuni katika Uwanja wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (NJIA), Rais Magufuli alisema siku moja walikamata almasi inayopita uwanja wa ndege ambayo walisema ilikuwa ya thamani ya dola za Marekani bilioni 14 lakini waliibaini ilikuwa ya tahamni ya zaidi ya dola bilioni 29.5. kwa safari moja pekee.
Post A Comment: