
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
Mbunge wa Mtama, Nape Nnauye amesema kuwa anafahamu Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu anayo mengi ya kuzungumza juu ya tukio la kupigwa risasi kwani gari lililotumika na washambuliaji ndilo gari ambalo baadhi ya wabunge walidai linawafuatilia.
"Hii gari imeripotiwa kufuatilia wabunge kadhaa hapa nikiwepo mimi, na tulisha ripoti gari hilo kwamba hatuelewi ni mtu gani ambaye anatufuatiliaga. sasa gari hiyo hiyo namba hizo hizo na idadi ya watu hao hao lakini hatua hazikuchukuliwa mpaka maswahibu yamemkuta mwenzetu ni wazi hili jambo ni kubwa na najua Lissu anayo mengi ya kutuambia". Nape
Nape amesema ingawa vyombo vya dola vitaendelea na kazi ya upelelezi lakini angependa kama Lissu akirudi kutoka kwenye matibabu azungumzie zaidi kwani hata siku alipozungumza na wanahabari kuhusu gari linalomfuatilia hakusema kwa undani.
"Mh. Lissu pamoja na dereva wake ninauhakika wana mengi ya kusimulia juu ya hili kwani tangu amelilalamikia siyo muda mrefu kutoka sasa. Na kwa vile tayari amejeruhiwa anaweza akatueleza kwa kina juu ya tukio hili" Nape .
Post A Comment: