
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
MKUU wa Gereza la Segerea amewekwa njia panda juu ya matibabu ya mfanyabiashara Harbinder Sethi Singh, huku ikimtaka kumpeleka katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ndani ya siku 14.
Amri hiyo ilitolewa jana na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, huku mkuu huyo wa gereza kutakiwa afike mahakamani kujieleza iwapo hatatekeleza agizo hilo.
Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi, alitoa amri hiyo baada ya wakili wa utetezi, Joseph Makandege, kuwasilisha maombi kwa mara ya nne kwamba mshtakiwa huyo bado anasumbuliwa na maradhi ya tumbo yanayosababishwa na puto alilowekewa.
Makandege alidai kuwa upande wa Jamhuri bado unaendelea kuidharau mahakama na kukiuka amri halali ya kuwataka kumpeleka mshtakiwa Muhimbili.
"Mheshimiwa Hakimu, upande wa Jamhuri unaitumia mahakama yako kuwakandamiza washtakiwa hasa wa kwanza (Sethi) anateseka kwa sababu wamekiuka amri halali ya kumpatia matibabu stahiki.
Kama wameshindwa kumhudumia mshtakiwa hakuna sababu ya kuendelea kuwatesa mahabusu mahakama yako ifute mashtaka ili washtakiwa wapate haki yao ya msingi hasa matibabu," alidai Makandege.
Hata hivyo, Wakili wa Serikali Mwandamizi, Leonard Swai, alidai kuwa upande wa Jamhuri unaomba mahakama iwape muda kwa ajili ya kushughulikia utaratibu wa kumpeleka mshtakiwa hospitali anayotaka.
" Mheshimiwa Hakimu, mahakama haitumiki kuwatesa washtakiwa, ilitoa amri kuhusu maombi ya utetezi lakini kuna utaratibu wa Jeshi la Magereza wa kutoa matibabu kwa mahahusu hata bila kuwa na amri yoyote," alidai Swai.
Swai alidai kuwa upande wa Jamhuri umejitahidi kuwasiliana na magereza namna ya kumpeleka Sethi Muhimbili na unaomba muda wa ziada wa kukamilisha utaratibu huo.
Hakimu Shaidi alisema mahakama yake ni sikivu imesikia maombi ya Jamhuri na kwamba mshtakiwa apelekwe Muhimbili ndani ya siku 14 .
"Mshtakiwa asipopelekwa Hospitali ya Muhimbili ndani ya siku 14, Mkuu wa Gereza la Segerea aje aileze mahakama kwa nini wameshindwa kumkamilishia huduma hiyo," alisema Hakimu Shaidi.
Alisema kesi hiyo itatajwa Oktoba 13, mwaka huu, na washtakiwa wataendelea kukaa mahabusu.
Mbali na Sethi, mshtakiwa mwingine ni James Lugemarila na wote wanakabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi na utakatishaji fedha.
Seth na Rugemarila wanakabiliwa na mashtaka 12 ya uhujumu uchumi kwa kula njama, kujihusisha mtandao wa uhalifu , kughushi, kutoa nyaraka za kughushi, kujipatia fedha kwa njia za udanganyifu, kutakatisha fedha na kuisababisha hasara ya dola za Marekani 22, 198,544.60 na Sh. 309,461,300,158.27.
Post A Comment: