
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi 🇵🇪🇵🇪
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
MBUNGE wa Singida Kaskazini (CCM), Lazaro Nyalandu, amesema Tanzania kwa sasa inahitaji Katiba Mpya na kushauri mihimili mitatu ya utawala iwe na mipaka.
Mihimili mitatu ya dola ni Serikali, Bunge na Mahakama ambayo kila mmoja una mamlaka yake katika utendaji na haiingiliani.
Mihimili hiyo kila mmoja una majukumu yake yaliyoainishwa vizuri kikatiba, ili kuhakikisha hakuna mwingiliano baina ya mmoja na mwingine kwa lengo la kuifanya iwe huru katika utendaji wao.
Juzi, katika ukurasa wake wa Twitter, Nyalandu alisema Tanzania inahitaji katiba mpya na kwamba mihimili ya utendaji wake iwekewe mipaka iliyo wazi.
“Tanzania inahitaji Katiba mpya… na kuwapo ‘checks and balances’ (uangalizi na usawa) kwa Serikali, Bunge na Mahakama,” alisema Nyalandu.
Mchakato wa kupata katiba mpya ulianza Aprili, 2012 baada ya Rais mstaafu Jakaya Kikwete kuwateua wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba walioongozwa na Jaji Joseph Warioba na makamu wake, Jaji Augustino Ramadhan.
Baada ya kukusanya maoni, Tume hiyo Machi 18, 2014 kupitia kwa Jaji Warioba iliwasilisha kwenye Bunge Maalum la Katiba.
Hatua iliyofuata ilikuwa kujadiliwa na Bunge, ili kuandika Katiba Mpya Inayopendekezwa na kazi hiyo ilifanyika na kukabidhiwa kwa Rais, lakini hadi sasa hakuna kilichoendelea baada ya hapo.
Post A Comment: