
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi 🇵🇪🇵🇪
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
MBUNGE wa Jimbo la Arusha Mjini, Godbless Lema, amempongeza Rais John Magufuli, kwa kutoa mchango wa Sh. Milioni 260, kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za polisi 13 waliounguliwa moto Septemba 27.
Akizungumza jana na waandishi wa habari ofisini kwake, Lema ambaye ni Waziri Kivuli wa Mambo ya Ndani, alisema tukio la kuunguliwa polisi moto nyumba zao ni la kusikitisha na kumshauri Rais awajengee polisi wote Arusha na mikoa mingine nyumba bora.
“Hawa polisi ni walinzi wetu na wanafanya kazi kubwa ya kutulinda, lakini nyumba zao hazistahili kuishi binadamu ni kama zizi la ng’ombe, namshauri rais atenge bajeti ya kuwajengea polisi ghorofa au nyumba za hadhi yao,” alisema.
Alisema polisi kulingana na kazi zao wanazofanya hawastahili kufanyiwa harambee ya kujengewa nyumba, bali inatakiwa serikali kuamua kuboresha nyumba zao na miundombinu yao.
Aidha, alisema anatamani kutoa msaada, lakini kwa hali ilivyo sasa, anafahamu hautapokelewa.
Pia alimshauri Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba kujitafakari kama anafaa kuendelea kuwapo katika nafasi yake kutokana na matukio yanayoendelea nchini ya utekwaji watu na kupigwa risasi.
“Ben Saanane ametekwa na mpaka leo hajulikani alipo, sasa watawezaje kufanya uchunguzi wa tukio la kupigwa risasi Mwanasheria Mkuu wa Chadema Tundu Lissu na kuwapata wahusika, wakati hao wengine hawajafahamu, ndio maana tunataka wachunguzi wa nje ya nchi, lakini ajitafakari kama anafaa au la,” alisema.
Post A Comment: