
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
KATIBU Mkuu wa Chama Cha Wananchi (CUF) Maalim Seif Sharif Hamad, amemuonya Msajili wa Vyama vya Siasa kuwa kamwe njama anazozifanya haziwezi kukiboa chama hicho.
Akizungumza na wanachama wa chama hicho katika mkutano mkuu wa wilaya ya Magharib A Unguja, Maalim Seif, alisema Msajili badala ya kuvilea vyama vya siasa, amekuwa akivibomoa hasa vile vyenye nguvu kikiwamo chama cha CUF.
βNjama anazozifanya Msajili wa Vyama vya Siasa kwa kushirikiana na Profesa Ibrahim Lipumba, kuibomoa CUF, kamwe hawezi wala hatoweza, wanachokifanya ni sawa na kutwanga maji katika kinu,β alisema.
Aidha, alisema njama hizo pia zimekuwa zikiungwa mkono na vyombo vya dola kwa kuwa kila anapoenda Lipumba kukihujumu chama hicho, amekuwa akilindwa na vyombo hivyo.
βHuu ni mpango wa dola, Lipumba yupo mbele tu na mimi nawaambieni wajumbe kuwa visa vyao vitazidi kipindi hiki kwa kuwa hivi sasa wana mpango wa kuhujumu matawi ya chama hiki ili wanaCUF waje juu wapate nafasi ya kuwakamata viongozi wa wao wakiamini kufanya hivyo haki haitorudi, lakini pia wana mpango wa kufungua matawi Zanzibar kinyume na utaratibu tuliojiwekea,β alidai.
Post A Comment: