
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi 🇵🇪🇵🇪
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
HATMA ya lini mshambuliaji Obbrey Chirwa ataanza kuitumikia Yanga, itajulikana leo baada ya kikao cha Kamati ya Maadili ya TFF ambacho kimemtaka nyota huyo kuhudhuria kikao hicho.
Uongozi wa Yanga umesema kuwa umepokea barua ya wito wa kuitwa Chirwa kwenye kikao cha Kamati ya Maadili ya TFF, ambayo itajadili suala lake la vurugu zilizotokea kwenye mchezo wa mwisho msimu uliopita dhidi ya Mbao FC katika Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.
Wakati hatma ya Chirwa ikisubiriwa, mshambuliaji Amissi Tambwe bado hali yake ya afya haijatengemaa na hivyo ataukosa mchezo wa Jumatano wa Ligi Kuu dhidi ya Njombe Mji.
Tambwe ambaye anasumbuliwa na maumivu ya mguu, hakucheza kwenye mchezo wa Ngao ya Jamii dhidi ya Simba na mchezo wa kwanza wa msimu mpya wa Ligi Kuu dhidi ya Lipuli ya Iringa, ambao walilazimisha sare ya bao 1-1 katika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na gazeti la Nipashe jana, Meneja wa timu hiyo, Hafidh Saleh, alisema Tambwe bado hajaanza mazoezi, hivyo hatokuwapo kwenye kikosi kitakachosafiri Jumapili kwenda Njombe kwa ajili ya mchezo wao na Njombe Mji.
“Tambwe hawezi kusafiri na timu, bado hajapona, na kuhusu Chirwa hatma yake itajulikana kesho [leo] baada ya kikao na TFF, tumepokea barua leo (jana) ikimtaka Chirwa kufika TFF kesho (leo) saa nane mchana,” alisema Saleh.
Aidha, alisema timu hiyo mbali na kumkosa Tambwe, pia itawakosa Beno Kakolanya, Geofrey Mwashiuya ambao nao ni majeruhi.
“Kakolanya na Mwashiuya bado hawajapona na wanaendelea na matibabu nao pia hawatacheza mchezo ujao dhidi ya Njombe Mji,” aliongezea kusema Saleh.
Alisema wanategemea kuondoka Dar es Salaam Jumapili asubuhi kuelekea Njombe tayari kwa mchezo wao wa pili msimu huu.
Post A Comment: