Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) lina mpango wa kupunguza muda wa mchezo wa mpira wa miguu, kuwa dakika 30 kila kipindi.


Bodi ya kimataifa ya soka duniani inatarajia kujadili pendekezo hilo linalolenga kuondoa upotezaji muda kwa makusudi, tabia inayofanywa wachezaji uwanjani.

Aidha waliopendekeza mpango huo wanasema kuwa mechi huchezwa kwa dakika 60 pekee kati ya 90 na muda uliosalia hutumiwa vibaya na wachezaji.

Pendekezo jingine ni wachezaji kutoruhusiwa kupiga mpira mara ya pili baada ya kipa kuupangua wakati wa penalti na iwapo penalti haikupigwa inavyostahili, mchezo utasitishwa na mpira wa adhabu kutolewa.

Mapendekezo mengine ni kama kuweka saa katika uwanja ambayo italingana na ile ya refa mbali pamoja na sheria mpya itakayoruhusu mchezaji kujipigia mpira au hata kutamba na mpira wakati anapopiga mpira wa adhabu.
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: