Utafiti mpya unaonyesha kuwapo kwa uhusiano kati ya unywaji wa pombe miongoni mwa wanawake na ongezeko la kupata na saratani ya matiti.


Kwa mujibu wa ripoti kutoka na mfuko wa utafiti wa saratani ni kuwa nusu glasi ya mvinyo au bia kwa siku huongeza uwezekano wa kupata saratani ya matiti.

Mbali na hayo, utafiti huo pia unaonesha kuwa mazoezi ya mara kwa mara huweza kusaidia kupunguza hatari ya kupata maradhi hayo ya saratani.

Inaelezwa kuwa saratani ya matiti ndiyo huwakumba zaidi wanawake nchini Uingereza huku mmoja kati ya wanawake wanane wakipatwa na ugonjwa huo katika maisha yao

Chanzo: BBC Swahili
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: